logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sri Lanka: Rais Gotabaya Rajapaksa ajiuzulu baada ya kutoroka Sri Lanka

• Serikali ya Singapore ilisema "aliruhusiwa kuingia kwa ziara ya kibinafsi".

image
na Radio Jambo

Burudani14 July 2022 - 19:08

Muhtasari


• Serikali ya Singapore ilisema "aliruhusiwa kuingia kwa ziara ya kibinafsi".

Gotabaya Rajapaksa amejiuzulu kama rais wa Sri Lanka baada ya kukimbilia Singapore kutokana na maandamano makubwa nyumbani kwake kupinga utawala wake.

Inaaminika alitaka kuondoka Sri Lanka kabla ya kuachia ngazi ili kuepusha uwezekano wa kukamatwa chini ya utawala mpya.

Aliwasili Singapore baada ya kwanza kuelekea Maldives Jumanne usiku. Taarifa zinasema ameandamana na mkewe na walinzi wawili.

Katika mji mkuu wa Colombo, waandamanaji walipokea taarifa za kujiuzulu kwake kwa vifijo na nderemo.

Serikali ya Singapore ilisema "aliruhusiwa kuingia kwa ziara ya kibinafsi".

Haijabainika iwapo Bw Rajapaksa atasalia au atahamia mahali pengine.

Gharama ya chakula, mafuta na bidhaa zingine za kimsingi imepanda na raia wa Sri Lanka wanakabiliw ana wakati mgumu.

"Hajaomba hifadhi na wala hajapewa hifadhi yoyote. Singapore kwa ujumla haitoi maombi ya hifadhi," Wizara ya mambo ya nje ya Singapore ilisema, ikithibitisha kuwasili kwa kiongozi huyo nchini humo.

Bw. Rajapaksa ambaye kama rais ana kinga ya kutoshtakiwa, inaaminika alitaka kuondoka Sri Lanka kabla ya kujiuzulu ili kuepusha uwezekano wa kukamatwa na utawala mpya.

Kaimu Rais Ranil Wickremesinghe leo Alhamisi aliweka amri ya kutotoka nje kwa siku ya pili ili kuzima maandamano.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved