logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Muigizaji maarufu wa Nigeria ahukumiwa kwa unyanyasaji kingono dhidi ya watoto

Mwaka jana, Bw Ominyika alikiri kumdhulumu mwathiriwa.

image
na Radio Jambo

Habari15 July 2022 - 05:25

Muhtasari


•Kesi hiyo imechukua mwaka huku upande wa mashtaka na utetezi wakiwasilisha ushahidi wao kwa nyakati tofauti mwaka jana.

•Makosa mawili ya unyanyasaji wa kijinsia yalitupiliwa mbali kutokana na kukosekana kwa ushahidi wa kutosha.

akipelekwa katika jela baada ya kuhukumiwa kifungo cha miaka mitano

Muigizaji maarufu nchini Nigeria siku ya Alhamisi amehukumiwa kifungo cha miaka mitano jela kwa kosa la kumdhalilisha kingono mtoto mdogo kati ya 2013 na 2014.

Kesi hiyo imechukua mwaka huku upande wa mashtaka na utetezi wakiwasilisha ushahidi wao kwa nyakati tofauti mwaka jana.

Kulingana na mawandishi wa BBC Rhoda Odhiambo ambaye alikuwa katika mahakama ya Lagos, akiwa amevalia fulana ya manjano na suruali ya jeans nyeusi, Bw Olarenwaju Ominyika almaarufu ‘baba Ijesha’ alisimama kizimbani huku hakimu akimhukumu kifungo gerezani.

Sio tena mtu huru, lakini mfungwa hakimu aliamua kwamba anafaa kutumikia kifungo cha miaka kumi na sita kwa jumla kwa mashtaka manne ambayo alipatikana na hatia.

Lakini kwa vile angetumikia vifungo vyote kwa wakati mmoja, ikawa miaka mitano.

Makosa mawili ya unyanyasaji wa kijinsia yalitupiliwa mbali kutokana na kukosekana kwa ushahidi wa kutosha.

Mwaka jana, Bw Ominyika alikiri kumdhulumu mwathiriwa.

Alisema mama wa mwathiriwa alimpigia simu na kumtaka awe sehemu ya utayarishaji wa filamu, ambapo ataonekana kuwa mwanaharakati wa kupinga unyanyasaji wa kijinsia kwa watoto.

Lakini hakimu alisema akiwa mtu mzima mwenye akili timamu, hakupaswa kumdhulumu mtoto, hata kama ni kwa ajili ya kuigiza.

Mwathiriwa na mamake hawakuwa mahakamani wakati uamuzi huo unasomwa.

Wanaharakati wa haki za wanawake na watoto wanasema uamuzi huo utakuwa mfano kwa yeyote anayenuia kumdhulumu mtoto.

Hata hivyo, mawakili wake wanapanga kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved