logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Serikali ya Uganda yapiga Marufuku Wasanii kutumbuiza wanafunzi Shuleni

"Walimu wakuu na Wakuu wa Shule zote za Msingi na Sekondari wanaonywa kutoajiri au kuruhusu yeyote kati ya "wasanii" hawa kufanya maonyesho shuleni'' Agizo kutoka katika waraka hiyo.

image
na Radio Jambo

Habari04 August 2022 - 06:14

Muhtasari


•Haya yanajiri baada ya mwezi uliopita Mbunge wa Tororo Sarah Acheing Opendi kuliambia bunge kuwa kiwango cha wanamuziki kueneza uasherati shuleni ni cha kutisha na hivyo akatoa wito wa kupigwa marufuku kwa wanamuziki wa kilimwengu kutumbuiza shuleni.

Mwanamuziki kwa jukua

Wizara ya Elimu na Michezo Uganda  imepiga marufuku mara moja kwa shughuli zozote zinazohusiana na  wanamuziki kutumbuiza wanafunzi  katika Shule za Msingi na Sekondari.

Marufuku hiyo ambayo inaanza kutumika mara moja itatekelezwa katika shule za msingi na sekondari za serikali na za kibinafsi.

Haya yamo katika waraka ambao ulitolewa kwa walimu wakuu na Wakuu wote wa shule na Dk Jane Okou kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara.

"Walimu wakuu na Wakuu wa Shule zote za Msingi na Sekondari wanaonywa kutoajiri au kuruhusu yeyote kati ya "wasanii" hawa kufanya maonyesho shuleni. Wasimamizi wa shule wanapaswa kuwajibika na kudii maagizo haya, yule ambaye atapatikana kuenda kinyume na hii maagizo atachukuliwa hatua''  Agizo kutoka katika waraka hiyo.

Wizara pia ilibainisha kuwa shughuli za ziada shuleni kwa kawaida kama vile michezo na uimbaji, vilabu vya mijadala, n.k na ikiwa shule zinahitaji kujiliwaza, basi zinaweza kushiriki katika maigizo ya kuigiza au kupanga matamasha.

Haya yanajiri baada ya mwezi uliopita Mbunge wa Tororo Sarah Acheing Opendi kuliambia bunge kuwa kiwango cha wanamuziki kueneza uasherati shuleni ni cha kutisha na hivyo akatoa wito wa kupigwa marufuku kwa wanamuziki wa kilimwengu kutumbuiza shuleni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved