logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tanzania yaonya dhidi ya kusambaza maudhui yanayounga mkono mapenzi ya jinsia moja

Tanzania imetoa onyo kwa wanaojihusisha na kusambaza maudhui mitandaoni ya uhusiano wa jinsia moja.

image
na Radio Jambo

Burudani12 September 2022 - 10:57

Muhtasari


•Waziri wa mawasiliano alisema ni kosa kisheria nchini Tanzania kwa mtu yeyote kusambaza maudhui hayo hata kama yanalenga kuelimisha.

Serikali ya Tanzania imetoa onyo kwa wanaojihusisha na kusambaza maudhui mitandaoni ikiwemo video fupi zinazohimiza uhusiano wa jinsia moja.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye aliyasema hayo jana Jumapili  jijini Dar es Salaam ambapo alisema kuwa  Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ilibaini kuwa baadhi ya watazamaji wa maudhui ya kulipia mtandaoni wamekuwa wakitazama na kusambaza maudhui hayo zikiwemo video kwenye mitandao ya kijamii. 

Nape alieleza kuwa uwepo wa huduma hizo zinazopatikana ulimwenguni zinawafanya watu kupokea tamaduni, mila na desturi kupitia picha jongefu wanazoangalia mtandaoni baada ya kulipia. 

Alisema ni kosa kisheria nchini Tanzania kwa mtu yeyote kusambaza maudhui hayo hata kama yanalenga kuelimisha, badala yake wanapotumiwa video hizo wafute na si kuzisambaza. 

Aidha alisema Serikali imepanga kuwachukua hatua kali kwa wanaoongoza makundi ya mitandao ya kijamii ambao wanachama wao wamekuwa wakishawishi kitendo hicho kwa kusambaza maudhui hayo. 

“Kiujumla anga letu la mtandao liko salama kwani TCRA wapo kazini kuhakikisha kuwa tunaendelea kuwa salama na hata inapotokea kuna maudhui hasi na yanayokiuka sheria, inachukua hatua stahiki kwa wanaohusika kwa kushirikiana na vyombo vya dola hasa jeshi la polisi,” alisema Nape. 

Nape amewahas wazazi, walimu na walezi kuwa wana wajibu wa kuwalinda watoto kutokana na maudhui yasiyofaa hasa yanayorushwa kwenye mitandao ya kijamii. 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved