logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais wa Ukraine Zelensky ahusika katika ajali ya gari lakini 'hakujeruhiwa sana'

Haya yanajiri baada ya Zelensky kutembelea mji uliokombolewa  wa Izyum.

image
na Radio Jambo

Habari15 September 2022 - 06:35

Muhtasari


• Gari la abiria liligongana na gari la rais na msafara wake katika mji mkuu wa Kyiv, Sergii Nykyforov alisema katika taarifa fupi.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amehusika katika ajali ya barabarani, msemaji wake amefichua.

Gari la abiria liligongana na gari la rais na msafara wake katika mji mkuu wa Kyiv, Sergii Nykyforov alisema katika taarifa fupi.

“Rais alifanyiwa uchunguzi na daktari, hakuna majeraha makubwa yaliyopatikana,” alisema.

Dereva wa gari lililogongana na msafara huo alitibiwa eneo la tukio na kukimbizwa kwenye gari la wagonjwa. 

Bw Nykyforov alisema mazingira yote ya ajali hiyo ya barabarani yalikuwa yanachunguzwa na maafisa wa kutekeleza sheria. Hakutoa maelezo zaidi.

Haya yanajiri baada ya Rais Zelensky, 44, kutembelea mji uliokombolewa  wa Izyum, kitovu muhimu cha usafirishaji kaskazini-mashariki mwa Ukraine, siku ya Jumatano.

Aliwashukuru wanajeshi walioshiriki katika mashambulizi ya haraka dhidi ya wavamizi wa Urusi, na kusimamia sherehe ya kupandisha bendera.

Katika siku za hivi karibuni, jeshi la Ukraine limerejesha sehemu kubwa ya eneo lililokaliwa, na kuwalazimu wanajeshi wa Urusi kurudi nyuma.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved