Mwanaume akamatwa baada ya kulisogelea jeneza la Malkia

Alikamatwa chini ya sheria ya utulivu wa umma na kupelekwa katika mahabusu.

Image: BBC

Mwanaume mmoja amekamatwa baada ya kulisogelea jeneza la Malkia Elizabeth II  kutoka kwenye msururu wa waombolezaji katika Westminster Hall.

Alikamatwa chini ya sheria ya utulivu wa umma  na kupelekwa katika mahabusu, Polisi imesema.

Tukio hilo lilitokea katika bunge  majira ya saa nne  za usiku Ijumaa , kulingana na taarifa ya polisi.

Matangazo ya video ya moja kwa moja  maalum kwa ajili ya tukio la umma kuutazama mwili wa Malkia yalikatizwa kwa kipindi kifupi wakati wa tukio hilo.

Taarifa ya makao makuu ya polisi -Scotland Yard ilisema : "Takriban saa nne za usiku Ijumaa tarehe 16 Septemba, maafisa  wa polisi wa ulinzi wa bunge na wa kidiplomasia walimkamata mwanaume katika Westminster Hall kufuatia usumbufu."

Msemaji wa bunge alisema: "Tunafahamu kuhusu tukio katika Westminster Hall,  ambapo mjumbe wa umma alitoka nje ya msururu na kuelekea kwenye jeneza.

"Kwa sasa ameondolewa kutoka katika ukumbi na msururu ulianza upya kusonga baada ya usumbufu mdogo."

 Mapema jioni, Mfalme Charles III aliungana na ndugu zake  Bintimfalme Anne, Mwanamfalme  Andrew na Mwanamfalme  Edward, katika mkesha wa maombolezo ndani ya ukumbi.

Marehemu Malkia Elizabeth II  atatazamwa na umma katika Westminster Hall hadi siku ya mazishi yake Jumatatu wiki ijayo. 

Baridi haikuwazuia waomblezaji kusimama kwenye misururu

Wakati hayo yakijiri misururu ya kuutazama mwili wa umma imeendelea usiku mzima mjini London, licha ya viwango vya joto kushuka hadi kufikia nyuzijoto 1. Baridi hiyo haikuwazuia maelfu ya watu kuendelea kusimama kwenye misururu kwa ajili ya kuutazama mwili wa Malkia.

Image: BBC

Masharti yawekwa kwa safari za ndege Jumatatu

masharti ya kuzuia safari za ndege  juu ya London na Windsor siku ya Jumatatu ijayo

 Mamlaka ya safari za ndege  (CAA) inasema hakuna ndege , pamoja na zisile zisizokuwa na rubani (droni) itakayoruhusiwa kupaa chini ya futi  2,500 (au mita 762) juu ya maeneo ambapo ibada itakuwa ikifanyika 

 CAA inasema marufuku hiyo – ambayo inajumuisha maputo madogo na  na tiara- ni muhimu kwa sababu za kiusalama