logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wahudumu 5 wa afya wameambukizwa ebola nchini Uganda

Wahudumu wa afya walisema wako kwenye mgomo hadi hali zao za kazi zitakapoboreshwa.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri28 September 2022 - 18:58

Muhtasari


  • Jumla ya watu ishirini na wanne wamethibitishwa kuambukizwa virusi hivyo nchini, watano kati yao wamefariki

Takriban wahudumu wa afya watano wamethibitishwa kuambukizwa virusi vya Ebola huku mlipuko huo ukiendelea kuenea katika eneo la kati nchini Uganda.

Dkt. Herbert Luswata katibu mkuu wa Chama cha Madaktari Uganda ameambia BBC kwamba wenzake waliambukizwa virusi hivyo katika hatua za kwanza za mlipuko huo wakati ufahamu ulikuwa mdogo na kwamba hawakuwa na vifaa vya kutosha vya kujikinga.

Watano hao kwa sasa wanapokea matibabu katika hospitali ya Mubende, kituo kikuu cha walioambukizwa Ebola.

Jumla ya watu ishirini na wanne wamethibitishwa kuambukizwa virusi hivyo nchini, watano kati yao wamefariki.

Chama cha wafanyikazi wa matibabu hapo awali kilitoa wito kwa maeneo yenye Ebola kuwekwa chini ya karantini ili kukomesha kuenea zaidi kwa ugonjwa wa virusi vya hemorrhagic.

Katika taarifa siku ya Jumanne, wafanyikazi wa matibabu waliofunzwa walisema hawatarejea kazini hadi wote watakapopimwa Ebola na wale waliopatikana wameambukizwa kutoa matibabu.

Wahudumu wa afya walisema wako kwenye mgomo hadi hali zao za kazi zitakapoboreshwa.

Rais Yoweri Museveni anatarajiwa kuhutubia nchi kuhusu mlipuko wa Ebola Jumatano usiku.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved