logo

NOW ON AIR

Listen in Live

China kufungua vituo vya Polisi Afrika ikiwemo nchini Tanzania

Vanguard imesema mpangilio wa China unaweza kuonekana kama shambulio dhidi ya uhuru wa eneo husika.

image
na Samuel Maina

Habari19 October 2022 - 07:57

Muhtasari


    China inadaiwa kufungua vituo vya polisi nchini Nigeria, Lesotho na Tanzania ili kudhibiti vitendo vya uhalifu vinavyofanywa na raia wake wanaoishi katika nchi hizo tatu za Afrika, tovuti inayomilikiwa na mtu binafsi ya Nigeria ya Vanguard imeripoti.

    Wakiwanukuu watetezi wa Usalama, Vanguard imesema mpangilio wa China unaweza kuonekana kama shambulio dhidi ya uhuru wa eneo husika.

    "Badala ya kushirikiana na serikali za mataifa hayo, [China] imeamua… kushirikiana na United Front linked , mashirika ambayo yako nje ya nchi katika mabara matano, kuanzisha mfumo mbadala wa polisi na mahakama ndani ya nchi tatu, na kuhusisha moja kwa moja mashirika hayo katika mbinu zisizo halali zinazotumiwa kuwasaka 'wakimbizi'," Watetezi hao wa usalama walisema walisema.

    Waliongeza kuwa mamlaka ya China, kati ya Aprili 2021 na Julai 2022, "imewashawishi" raia 230,000 kurejea China kujibu mashtaka ya jinai kuhusu mawasiliano ya simu na ulaghai wa jumla.

    Pia ilisema serikali ya China ilipiga marufuku raia wake kuhamia nchi tisa ambazo hazikutajwa kwa makosa ya "udanganyifu mkubwa, ulaghai wa simu na uhalifu wa mtandao".


    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved