logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mfahamu jamaa ambaye mlo wake ni chuma,glasi,wembe,misumari

Tangu Mwaka wa 1966 alikuwa amekula baiskeri 18, toroli 15, seti saba za Runinga

image
na Radio Jambo

Yanayojiri04 November 2022 - 10:16

Muhtasari


• Kufikia mwaka wa 1997, alikuwa amekula karibu tani tisa za chuma.

Mwanamume mmoja Mfaransa aliacha dunia nzima ikisemezana baada ya kuingia kwenye vitabu vya rekodi za Guinness kutokana na tabia yake ya kula chuma kama chakula chake.

Jamaa huyo anayefahamika kama Michel Lotito aliwekwa kwenye Guinness Book of Records baada ya kusemekana kuwa alikuwa akila chuma na glasi tangu alipokuwa miaka 9.

Kuta za tumbo la Michel zilikuwa nene mara mbili kuliko za mtu wa kawaida.

Kulingana na chapisho kwenye ukurasa wa Guinness Book of World Records madaktari walimpima Lotito tumboni mwake na mashine ya eksirei na  kusemekana kuwa, mlo wake usio ya kawaida ulitokana na ugonjwa unaoitwa pica.

Ugonjwa huo hufaonya mtu kutamani vyakula ambavyo si vyakula kawaida. Iliripotiwa kuwa Lotito anauwezo wa kula gramu 900 za chuma kwa siku.

Tangu utotoni mwake alikuwa akiwatumbuiza watu jukwani walioshangazwa na tabia yake ya kula vitu vinavyoongopesha kama ile nyembe,misumali,nati,vijiko na vinginevyo.

Tangu Mwaka wa 1966 alikuwa amekula baiskeri 18, toroli 15, seti saba za Runinga, taa za nyumba, ndege ndogo aina ya Cessna na kompyuta.

Kufikia mwaka wa 1997, alikuwa amekula karibu tani tisa za chuma.

Imepita miaka 10 tangu kifo cha Lotito, lakini hakuna aliyeweza kushinda rekodi yake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved