Mzozo wa Ukraine: Urusi yakamilisha zoezi la kuondoa vikosi vyake Kherson

Urusi imesema kwamba kuondoa vikosi Kherson haimainishi kutakua na mabadiliko, bado ni eneo lake.

Muhtasari

• Ilikuwa siku ya Jumatano ambapo wakuu wa jeshi la Urusi walitangaza kuwa wanaondoka kutoka upande huo wa mto.

Image: BBC

Habari za hivi punde ni kuwa Urusi imeonda vikosi vyote kutoka mji wa Kherson. Asubuhi nzima, picha zimeonekana kwenye mitandao ya kijamii zikionyesha sehemu kadhaa zilizoharibiwa kwenye daraja pekee la barabara nje ya Kherson.

Hilo liliwafanya wanablogu wanaofuatilia kwa karibu vita hivyo kusema kujiondoa kwa Urusi kutoka ukingo wa magharibi wa mto Dnipro kumekwisha. Sasa wizara ya ulinzi huko Moscow, iliyotajwa na shirika la habari la Tass, imethibitisha kwamba wanajeshi wote wa Urusi kwenye ukingo wa magharibi wamevuka upande mwingine.

Ilikuwa siku ya Jumatano ambapo wakuu wa jeshi la Urusi walitangaza kuwa wanaondoka kutoka upande huo wa mto.

Uamuzi wa kurudi nyuma ni pigo kubwa kwa jeshi la Urusi katika kukabiliana na shambulio la Ukraine.

Rais Vladimir Putin hakushiriki katika tangazo hilo la televisheni. Wizara hiyo ilisema Ijumaa kwamba hakukuwa na hasara ya wafanyikazi, silaha au vifaa vya kijeshi na kwamba hakuna vifaa vilivyoachwa nyuma.

Image: BBC

Kremlin bado inachukulia eneo la Kherson kuwa sehemu ya Urusi. Na haioni chochote cha kufedhehesha kutokana na kitendo cha kuondoa vikosi vyake kutoka eneo la Kherson.

Msemaji wa rais wa Urusi Dmitry Peskov alisema kuwa kuondolewa kwa wanajeshi wa Urusi kutoka Kherson hadi benki ya kushoto ya Dnieper hakutabadilisha hali ya eneo la Kherson lililoshikiliwa na Urusi.

"Hili ni somo la Shirikisho la Urusi, hali hii inafafanuliwa kisheria na kulindwa. Hakuna na hawezi kuwa na mabadiliko yoyote hapa," aliwaambia waandishi wa habari.

Peskov alikataa kujibu swali kutoka kwa waandishi wa habari kuhusu jinsi Vladimir Putin alichukua ripoti ya Jenerali Sergei Surovikin kuhusu hali ya Kherson na uamuzi wa Waziri wa Ulinzi Sergei Shoigu kuondoa kikundi cha kijeshi cha Urusi kutoka kwa jiji hilo.

"Kulikuwa na [uamuzi] wa Waziri wa Ulinzi, kwa hivyo nakuomba uwasiliane na Wizara ya Ulinzi, sina la kusema juu ya mada hii," Peskov alisema.

Akijibu swali kutoka kwa BBC, Peskov alisema kuwa Kremlin haioni kuwa ni fedheha kuondoka kutoka Kherson.