logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Idadi ya watu duniani, bilioni 8, China yaongoza India ni ya pili

Kulingana na UNFPA India itaipiku China kwa idadi ya watu ifikapo mwisho wa 2023 .

image
na Radio Jambo

Habari15 November 2022 - 07:39

Muhtasari


• Idadi hiyo imeripotiwa kuongeza baada ya watu bilioni 1 kuongezeka kwa kipindi cha miaka 12 ailiyopita.

• India imeripotiwa kukaribia kuishinda China kwa idadi ya watu ifikapo 2023.

Dunia yafikisha idadi ya watu bilioni 8

Jumanne Novemba 15, 2022 dunia imeripotiwa kufikisha idadi ya watu bilioni 8 baada ya kuongezeka kwa zaidi ya watu bilioni moja kwa kipindi cha miaka 12 ambayo imepita.

Kulingana na utafiti wa Shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu Idadi ya Watu (UNFPA) India itaipiku China kwa idadi ya watu ifikapo mwisho wa 2023 .

UNFPA ilisema kuongezeka kwa idadi ya watu kwa kiwango cha juu ni ishara ya kuimarika kwa sekta ya afya duniani.

"Dunia yetu sasa ni nyumbani kwa watu bilioni 8 hivyo ni kumaanisha kuna Matumaini bilioni 8,ndoto bilioni 8 na majukumu bilioni  8" UNFPA iliandika kwenye Twitter.

Ripoti ya UNFPA inasema India inakadiriwa kuipita China kama nchi yenye watu wengi zaidi duniani mwaka wa 2023.

Ripoti ya matarajio ya idadi ya watu ilisema kwamba idadi ya watu nchini India itafikia bilioni 1.412 mwaka wa 2022, ikilinganishwa na Uchina yenye bilioni 1.426.

India inakadiriwa kuwa na idadi ya watu bilioni 1.668 mnamo 2050, mbele ya watu bilioni 1.317 wa Uchina kufikia katikati ya karne.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved