logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hofu ya Ebola yafanya Uganda kufunga shule mapema kwa likizo ya Krismasi

Pia inakinzana na msimamo rasmi wa serikali kwamba hali imedhibitiwa.

image
na Radio Jambo

Burudani25 November 2022 - 10:50

Muhtasari


  • Katika miezi miwili iliyopita watu 55 wamekufa na virusi hivyo - na kuna uwezekano wa vifo 22 vya Ebola kabla ya mlipuko huo kutangazwa rasmi mnamo 20 Septemba

Krismasi huenda inakuja mapema kwa wanafunzi nchini Uganda hukumamilioni yao wakirejea nyumbani mapema kwa likizo ya shule siku ya Ijumaa.

Hata hivyo uamuzi wa kufungwa kwa shule kote nchini wiki mbili kabla ya mwisho wa muhula umechukuliwa ili kuzuia kuenea kwa Ebola, huku nchi hiyo ikiendelea kupambana na moja ya milipuko yake mbaya zaidi.

Pia inakinzana na msimamo rasmi wa serikali kwamba hali imedhibitiwa.

Katika miezi miwili iliyopita watu 55 wamekufa na virusi hivyo - na kuna uwezekano wa vifo 22 vya Ebola kabla ya mlipuko huo kutangazwa rasmi mnamo 20 Septemba.

Baadhi ya wataalam wameelezea kutoridhishwa kwao na hatua ya kufungwa kwa shule, wakisema kuwa kuwaweka wanafunzi ndani kwa wiki nyingine mbili itakuwa njia bora ya kukomesha kuenea kwa ugonjwa huo hatari.

Ebola ni maambukizi ya virusi ambayo husambazwa kupitia maji maji ya mwili wa mgonjwa.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved