logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mfanyibiashara wa kiume wa miaka 25 afariki ndani ya loji akiwa na mpenziwe

Kifo wakati wa kujamiiana kwa maelewano kinaweza kutokea kwa sababu kadhaa.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri31 January 2023 - 09:11

Muhtasari


• Musstafa alifariki Januari 25 mwendo wa saa tisa alasiri kutokana na kushindwa kupumua.

Polisi nchini Uganda katika kanda ya Magharibi mwa Mto Nile wanachunguza kisa ambapo mwanamume mmoja aliyetajwa kama mfanyibiashara kufariki ndani ya chumba cha kulala wageni saa chache baada ya kuingia hapo na mpenzi wake wa kike.

Marehemu aliyetambuliwa kwa jina Ali Musstafa ni mfanyibiashara maarufu katika wadi ya Kenya wilayani Arua nchini humo na anadaiwa kufariki akiwa anavunja amri ya saba na mpenzi wake ndani ya gesti.

“Mwathiriwa alianguka na kufia chumbani. Msichana huyo alienda na kuwajulisha wasimamizi wa hoteli ambao mara moja walitoa taarifa kwa polisi wa Arua. Tukio hilo lilitembelewa na kurekodiwa vizuri, hakuna chembe ya dawa, sumu au athari zingine za mwili zilizopatikana kwenye eneo la tukio. Mwili ulihamishwa hadi Hospitali ya Rufaa ya Arua na kufanyiwa uchunguzi,” msemaji wa Polisi, SCP Fred Enanga alinukuliwa na jarida la Monitor nchini humo.

Kulingana naye, Musstafa alifariki Januari 25 mwendo wa saa tisa alasiri kutokana na kushindwa kupumua kabla ya mwili wake kuchukuliwa kutoka chumba cha hoteli na kufanyiwa uchunguzi wa maiti.

"Kifo wakati wa kujamiiana kwa maelewano kinaweza kutokea kwa sababu kadhaa, ambazo ni pamoja na mkazo wa kimwili wa shughuli au kwa sababu ya hali zisizo za kawaida," SCP Enanga aliongeza.

Tukio hili linakuja wiki moja baada ya tukio sawia kuripotiwa jijini Nairobi baada ya mwanamume mzee wa miaka 71 kufariki kwenye gesti akiwa na kidosho wa miaka 22.

Inaarifiwa kuwa kidosho huyo aliwataarifu watu wa gesti hilo baada ya mzee huyo kupata matatizo ya kupumua, gari liliitwa kumpeleka katika hospitali ya Agha Khan lakini alifariki kwa bahati mbaya.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved