Sanamu yenye mfano wa kichwa cha binadamu na mwili wa mnyama yagunduliwa nchini Misri

Sanamu yenye muundo wa mnyama na binadamu ilipatikana nchini Misri.

Muhtasari

•Ugunduzi huo ulifanywa katika upande wa mashariki wa Hekalu la Dendera huko Qena, ambapo uchimbaji bado unaendelea. Sphinxes ni viumbe vya mara kwa mara katika hadithi za tamaduni za kale za Misri, Kiajemi na Kigiriki. Mfano wao mara nyingi hupatikana karibu na makaburi au majengo ya kidini.

Sanamu mpya yenye umbo la kichwa cha binadamu na mwili wa mnyama kwa jina Sphynx imegunduliwa nchini Misri - lakini hii inadhaniwa kuwa ya Kirumi. Sanamu hiyo yenye tabasamu na mabaki ya kaburi lilipatikana wakati wa misheni ya uchimbaji huko Qena, mji wa kusini mwa Misri kwenye ukingo wa mashariki wa Mto Nile.

Madhabahu hayo yalikuwa yamechongwa kwa mawe ya chokaa na yalikuwa na jukwaa la ngazi mbili, Mamdouh Eldamaty, waziri wa zamani wa mambo ya kale na profesa wa Egyptology katika Chuo Kikuu cha Ain Shams, alisema katika taarifa Jumatatu kutoka wizara ya utalii na mambo ya kale ya Misri.

Bonde la ngazi na tofali za kuhifadhi maji zilipatikana ndani. Bonde hilo, linaloaminika kuwa la zamani za enzi ya Byzantine, lilikuwa na sanamu ya sphinx yenye tabasamu, iliyochongwa kutoka kwa chokaa.

Eldamaty alielezea sanamu hiyo kuwa na sifa za uso wa kifalme. Ilikuwa na tabasamu laini na dimples mbili. Pia alikuwa amevalia nemes kichwani mwake - kitambaa chenye milia kilichovaliwa kitamaduni na mafarao wa Misri ya kale, chenye ncha ya umbo la nyoka au "uraeus." 

 Timu kutoka Chuo Kikuu cha Ain Shams iligundua sphinx ndogo katika mji wa kusini mwa Misri wa Qena. Gena, Misri Stela ya Kirumi yenye maandishi ya hieroglyphic na demotic kutoka enzi ya Kirumi ilipatikana chini ya sphinx.

Profesa huyo alisema kwamba sanamu hiyo inaweza kuwakilisha Maliki Mroma Claudius, maliki wa nne wa Roma aliyetawala kuanzia mwaka wa 41 hadi 54, lakini akabainisha kwamba uchunguzi zaidi unahitajika ili kuthibitisha mmiliki na historia ya muundo huo.

Ugunduzi huo ulifanywa katika upande wa mashariki wa Hekalu la Dendera huko Qena, ambapo uchimbaji bado unaendelea. Sphinxes ni viumbe vya mara kwa mara katika hadithi za tamaduni za kale za Misri, Kiajemi na Kigiriki. Mfano wao mara nyingi hupatikana karibu na makaburi au majengo ya kidini.

Sio kawaida kwa sanamu mpya za sphinx kupatikana Misri. Lakini sphinx maarufu zaidi nchini, Sphinx Mkuu wa Giza, alianzia karibu 2,500 BC na inawakilisha Farao wa kale wa Misri Khafre. Eldamaty, ambaye pia ni rais wa chuo kikuu, alisema katika taarifa tofauti kwenye tovuti ya chuo hicho kuwa hii ni misheni ya kwanza ya Misri kufika eneo la Dendera.

Kazi huko itaendelea kwa misimu mingi ijayo, Eldamaty alisema, huku uchimbaji kwenye tovuti ukiahidi kuongeza mengi kwenye historia ya ustaarabu wa Misri katika enzi za Ugiriki na Warumi.