logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Museveni kujadili na wabunge kuhusu muswada dhidi ya mapenzi ya jinsia moja

Mkutano huo utafanyika katika Ikulu ya Entebbe

image
na Radio Jambo

Yanayojiri20 April 2023 - 10:57

Muhtasari


  • Sheria iliyopendekezwa imevuta hisia kimataifa, huku Marekani ikitishia kuiwekea Uganda vikwazo iwapo muswada huo utapitishwa kuwa sheria.

Rais wa Uganda Yoweri Museveni anatazamiwa kukutana na wabunge wa chama tawala cha National Resistance Movement (NRM) siku ya Alhamisi kujadili muswada 'tata' wa kupinga mapenzi ya jinsia moja uliopitishwa na bunge mwezi uliopita.

Mkutano huo utafanyika katika Ikulu ya Entebbe, kwa mujibu wa taarifa ya mwenyekiti wa kikao cha wabunge wa NRM, Denis Obua.

Wabunge wote wanatakiwa kupima Covid-19 kabla ya mkutano, tovuti ya serikali ya New Vision iliripoti.

Muswada huo, ambao vyombo vya habari vya ndani vinasema kuwa Bw Museveni huenda akatia saini kuwa sheria, utamshuhudia mtu yeyote anayejihusisha na vitendo vya mapenzi ya jinsia moja akikabiliwa na kifungo cha miaka 20 jela na hukumu ya kifo kwa wafungwa wa vitendo hivyo uliokithiri.

Sheria iliyopendekezwa imevuta hisia kimataifa, huku Marekani ikitishia kuiwekea Uganda vikwazo iwapo muswada huo utapitishwa kuwa sheria.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved