Mafuriko yakumba mji katikati mwa Somalia

Watu walilazimika kujificha chini ya miti baada ya mto Shebelle kuvunja kingo zake,

Muhtasari
  • Umoja wa Mataifa unaonya kuwa mafuriko yanaweza pia kuukumba mji wa Bulo Burde, umbali wa kilomita 110 (maili 68).
Image: BBC

Takriban watu 250,000 katikati mwa Somalia wamelazimika kuyahama makazi yao baada ya maji mafuriko kusomba mji wa Beledweyne.

Watu walilazimika kujificha chini ya miti baada ya mto Shebelle kuvunja kingo zake,

Asilimia 99 ya watu wanaoishi katika mji huo na maeneo ya karibu hawana makazi, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jimbo la Hirshabelle Abdirahmaan Dahir Gure aliambia BBC Somali.

Umoja wa Mataifa unaonya kuwa mafuriko yanaweza pia kuukumba mji wa Bulo Burde, umbali wa kilomita 110 (maili 68).

Mabadiliko ya hali ya hewa yanaaminika kuwa chanzo kikuu cha mafuriko hayo.

Kulingana na maafisa wa serikali ya Somalia, mvua kubwa iliyonyesha nchini Somalia na sehemu ya juu ya miinuko ya Ethiopia ilisababisha mafuriko ambayo yalisomba nyumba, mazao na mifugo.

Somalia ndiyo inaanza kupata nafuu kutokana na ukame mbaya zaidi kuwahi kutokea katika miongo kadhaa baada ya kukosa mvuo kwa misimu mitano mfululizo, na kutishiakutokea kwa janga la kibinadamu.

Kulingana na Umoja wa Mataifa, mvua hiyo inahuisha vyanzo vya maji na kusaidia mimea kukua lakini mvua nyingi zaidi inahitajika ili kupunguza athari za ukame wa hivi majuzi. Mvua nyingi pia huongeza hatari ya mafuriko.