logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nitasambaza silaha kwa Urusi - asema Julius Malema wa Afrika Kusini

Serikali ya Afrika Kusini imekana kuidhinisha usafirishaji wowote wa silaha kwenda Urusi.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri24 May 2023 - 10:23

Muhtasari


  • "Nitaenda zaidi ya urafiki na Urusi.Katika vita, nitaungana na Urusi na hata nitasambaza silaha,” Bw Malema alimwambia Stephen Sackur wa HARDtalk.

Kiongozi wa chama cha Economic Freedom Fighters (EFF), chama cha tatu kwa ukubwa cha kisiasa nchini Afrika Kusini, amesema "atasambaza silaha kwa Urusi" kwa sababu Moscow iko "katika vita na ubeberu".

Katika mahojiano na BBC mjini Johannesburg, Julius Malema alisisitiza kuwa "Afrika Kusini ni mshirika wa Urusi" na kwamba msimamo wa serikali ya ANC wa kutojihusisha na siasa unahusu vita vya Ukraine pekee.

"Nitaenda zaidi ya urafiki na Urusi.Katika vita, nitaungana na Urusi na hata nitasambaza silaha,” Bw Malema alimwambia Stephen Sackur wa HARDtalk.

EFF pia inaitaka Afrika Kusini kujiondoa katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).

Mahakama ya ICC imetoa hati ya kukamatwa kwa Vladimir Putin kwa tuhuma za uhalifu wa kivita lakini Bw Malema ameahidi kuzuia jaribio lolote la kumkamata rais huyo wa Urusi iwapo atahudhuria mkutano wa kilele wa Brics mwezi ujao mjini Cape Town.

Bw Malema alitoa maoni hayo kufuatia mzozo wa kidiplomasia ambapo balozi wa Marekani nchini Afrika Kusini alidai kuwa silaha na risasi zilipakiwa kwenye meli ya Urusi iliyotia nanga nchini humo Desemba mwaka jana.

Serikali ya Afrika Kusini imekana kuidhinisha usafirishaji wowote wa silaha kwenda Urusi.

 

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved