logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanafunzi 400 waliokuwa wanasomea kozi ya uganga wa jadi wahitimu Tanzania

"Tunajaribu kwa njia zote kuendeleza mila sahihi,” mbunge huyo alisema.

image
na Radio Jambo

Habari19 September 2023 - 07:04

Muhtasari


• Mbunge wa eneo hilo aliyekuwa mmoja wa waliohudhuria kuhafili kwao alisema kuwa watajaribu kadri ya uwezo wao kupeleka somo la kitamaduni shuleni katika mtaala mpya.

Mahafali wa uganga

Taifa la Tanzania limeingia katika vitabu vya historia kwa kutoa kundi la kwanza kabisa la wanafunzi ambao walikuwa wanasomea kozi ya uganga wa kienyeji.

Kwa mujibu wa Ayo TV, chuo cha uganga wa jadi cha Modesta kilichopo wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga kimekuwa cha kwanza kabisa kutoa wahitimu wasiopungua 400 ambao walikuwa wanaandaliwa kwa mafunzo kabambe ya uganga wa kiasili.

Mahafali hayo yalihudhuriwa na umati wa watu Zaidi ya elfu moja kushuhudia kufuzu kwa wanafunzi hao ambao walipitia mafunzo ya uganga kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Mbunge wa jimbo la Kahama, Jumanne Kishimba alitoa wito kwa serikali kukumbatia mafunzo hayo ya asili akisema kuwa ni sehemu ya tamaduni na wala hakuna mila, destruri na tamaduni zilizo potovu.

“Sasa hivi kwenye mtaala mpya wa elimu, tunapeleka suala la utamaduni shuleni na mimi ndiye nilikuwa nalipigania sana kwamba jamani tunahangaika. Mjini tunasema sijui tunaugua msongo wa mawazo, matatizo ya akili, sasa mbona kijijini hawaugui huo msongo wa mawazo? Kwa nini tusiende kwao tukawauliza kama nyinyi hamuugui ina maana hizi dawa mnazo. Tunajaribu kwa njia zote kuendeleza mila sahihi,” mbunge huyo alisema.

Taifa la Tanzania kwa muda mrefu limekuwa likijulikana kwa mila ya uganga wa kiasili ambao wengi wanaumini na vile vile kuuambatanisha na matukio ya ushirikina na uchawi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved