logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Dar es Salaam yapiga marufuku biashara za masaji na utingishaji makalio kwa vipusa

Mwaka jana pia Nairobi ilichukua hatua ya kupiga marufuku vilabu vya kelele.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri01 November 2023 - 09:30

Muhtasari


• RC Chalamila alitoa tamko lake kuhusu kuenea kwa vilabu vya starehe ambavyo vinapiga miziki ya kuleta kero.

Dar es Salaam wapiga marufuku masaji

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam nchini Tanzania Albert Chalamila amepiga marufuku biashara za kutoa huduma za masaji au ukandaji lakini pia mwenendo wa kina dada kutembea mitaani na katika sehemu za starehe wakitingisha makalio yao.

Akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wakuu wa wilaya zote katika mkoa huo mkubwa nchini humo, Chalamila alilalamika vikali kwamba baadhi ya biashara hizo ingawa aina leseni za kuhudumu, lakini zimemomonyoa maadili mazuri ya raia wa taifa hilo ambao wengi ni wahafidhina.

“Ni kweli ni mifumo ya kutoa leseni ila wakati Fulani hamuangalii biashara ambayo inaweza kuwa na athari katika jamii zinazotuzunguka. Kwa mfano juzi mumeona kuna picha inasagaa ya masaji wadada wanatikisa makalio yao kwenye maji sijui nini ile wanatoa mapofu. Hili linahitaji wakuu wa wilaya, madubwasha yote ya aina hiyo ambayo yanakiuka misingi ya maadili tuliyo nayo, mkazifunge zile biashara haraka, na mkazifunge kweli,” RC Chalamila alisema.

Kando na kufungwa kwa madubwasha ya masaji na kutingisha makalio, RC Chalamila alitoa tamko lake kuhusu kuenea kwa vilabu vya starehe ambavyo vinapiga miziki ya kuleta kero.

“Lakini hali ya sasa na kelele imezidi. Lazima tuwafundishe kuondokana na ushamba. Kelele nyingi hizi kwenye baa ni ushamba. Tukawape elimu ya miziki yao iishie kwa waliofuata miziki. Sasa hivi watu wengi wanalalamika, lakini ukiangalia wale wenye baa wana leseni. Katika hili, wakuu wa wilaya tufanye vikao na wamiliki wa baa,” alisema RC Chalamila.

Hatua hii inafuatia ikiwa ni mwaka mmoja tu baada ya uongozi wa Nairobi kupitia kwa gavana Sakaja pia kutoa tangazo la kufungwa kwa baa ambazo zimo kwenye sehemu za makazi.

Sakaja alilazimika kuchukua hatua hiyo kufuatia malalamishi kutoka kwa baadhi ya wakazi wa maeneo ambako vilabu vilikuwa vinapiga miziki yenye kero usiku kucha na kuwanyima usingizi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved