Abiria afungua mlango wa ndege na kutembea juu ya bawa

Jamaa amekamatwa nchini Mexico baada ya kufungua mlango wa dharura wa ndege na kutembea juu ya bawa.

Muhtasari

•Jamaa huyo alichukua hatua baada ya ndege hiyo iliyokuwa ikielekea Guatemala City kukwama kwa saa nyingi kwenye lami bila kiyoyozi wala maji kwa abiria.

•Haijabainika iwapo mwanamume huyo atasalia kizuizini - au ni mashtaka gani anaweza kukabiliwa nayo.

Image: BBC

Mwanamume mmoja amekamatwa nchini Mexico baada ya kufungua mlango wa dharura wa ndege na kutembea juu ya bawa.

Mwanamume huyo alichukua hatua baada ya ndege hiyo iliyokuwa ikielekea Guatemala City kukwama kwa saa nyingi kwenye lami bila kiyoyozi wala maji kwa abiria.

Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mexico ulisema hakuna madhara yoyote yaliyotokea, lakini abiria huyo amefikishwa kwa polisi.

Abiria wenzake, hata hivyo, wameandika taarifa ya pamoja, wakisema mtu huyo aliungwa mkono na kila mtu.

Tukio hilo lilitokea Alhamisi iliyopita, mwendo wa saa 11:30 - takriban saa tatu baada ya ndege ya Aeromexico kupangwa kusafiri kutoka Mexico City.

Ucheleweshaji huo ulisababishwa na suala la matengenezo, ripoti ya tukio ilisema.

Iliendelea kueleza kuwa kubadilishwa kwa ndege kumekuwa muhimu baada ya abiria huyo ambaye hajatambuliwa kuunga mkono kwa kauli moja na wenzake.

Haijabainika iwapo mwanamume huyo atasalia kizuizini - au ni mashtaka gani anaweza kukabiliwa nayo.

Abiria waliokasirika, hata hivyo, walichukulia tukio hilo kwa mtazamo tofauti.

"Abiria wote kwenye ndege kutoka CDMX [Mexico City] kwenda Guatemala [ndege] AM 0672 wanasema kwamba abiria aliyefungua dirisha la dharura alifanya hivyo kwa ajili ya ulinzi wa kila mtu, kwa msaada wa kila mtu, kwa sababu kuchelewa na ukosefu wa hewa ilisababisha hali hatari kwa afya ya abiria," barua iliyoandikwa kwa mkono na abiria wenzake inasomeka.

"Aliokoa maisha yetu," waliandika - na kuongeza majina na saini zao kwenye barua iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii