logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msako waendelea kuwatafuta wanasoka wa Morocco waliopotea baharini

Huduma za dharura ziliwaokoa watu watatu baada ya kisa hicho, lakini wachezaji wakuu Abdellatif Akhrif, 24, na Salman El-Harrak, 18, hawajapatikana

image
na SAMUEL MAINA

Habari09 July 2024 - 04:22

Muhtasari


  • •Huduma za dharura ziliwaokoa watu watatu baada ya kisa hicho, lakini wachezaji wakuu Abdellatif Akhrif, 24, na Salman El-Harrak, 18, hawajapatikana.

Klabu ya Morocco Ittihad Tanger imeiambia BBC kuwa msako unaendelea kuwatafuta wanasoka wawili waliotoweka katika pwani ya kaskazini mwa nchi hiyo ya Mediterania siku ya Jumamosi.

Wahudumu watano wa Ligi Kuu ya Morocco wanashiriki katika msako wa meli ya kifahari iliyokodishwa katika eneo la mapumziko la ufuo la M'diq - kaskazini mwa jiji la Tetouan, waliyokuwa wakisafiria.

Huduma za dharura ziliwaokoa watu watatu baada ya kisa hicho, lakini wachezaji wakuu Abdellatif Akhrif, 24, na Salman El-Harrak, 18, hawajapatikana.

Oussama Aflah, Soumaimane Dahdouh na Abdelhamid Maali, mchezaji wa kimataifa wa Morocco wa kikosi cha vijana wenye chini ya umri wa miaka 20, waliokolewa baada ya kuwa baharini kwa saa kadhaa.

Aflah namesajiriwa na klabu, wakati Dahdouh na Maali walikuwa wanakichukuliwa kuwa ni wachezaji wazuri wa timu wa akiba.

Rais wa Ittihad Tanger, Mohamed Cherkaoui alithibitisha kuwa "utafutaji wa wachezaji waliopotea bado unaendelea".

Pia amewataka mabaharia na mashabiki kwenye mitandao ya kijamii kuendelea kuwa makini na taarifa wanazotoa kuhusu wawili hao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved