logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maafisa wa serikali waliorekodiwa wakishiriki mapenzi kufutwa kazi;.

Zaidi ya wanawake 400 wanaripotiwa kushiriki mapenzi na mkurugenzi mkuu wa ANIF nchini Equatorial Giuinea katika sehemu tofauti tofauti ikiwemo afisi za serikali

image
na Brandon Asiema

Kimataifa05 November 2024 - 13:05

Muhtasari


  • Makamu wa rais wa Equitorial Guinea Teodoro Obiang Nguema amesema kuwa serikali ya nchi hiyo itawafuta kazi maafisa na watumishi wote wa umma wa taifa hilo ambao ni miongoni mwa wanawake waliorekodiwa katika sakata ya ngono.
  • Engonga alionekana akifanya mapenzi na wake wakiwemo mke wa mkuu wa ulinzi wa rais wa nchi hiyo, mtoto wa mkuu wa jeshi la polisi, mke wa mwanasheria mkuu, binamu yake, mke wa mlinzi wake kati ya wanawake wengine.

caption

Makamu wa rais wa Equitorial Guinea Teodoro Obiang Nguema amesema kuwa serikali ya nchi hiyo itawafuta kazi maafisa na watumishi wote wa umma wa taifa hilo ambao ni miongoni mwa wanawake waliorekodiwa katika sakata ya ngono na Mkurugenzi mkuu wa shirikala kitaifa la  upelelezi wa fedha (ANIF) la nchini Equitorial Guinea.


Zaidi ya wanawake 400 wanaripotiwa kushiriki mapenzi na mkurugenzi huyo mkuu katika sehemu tofauti tofauti ikiwemo afisi za serikali na nyumbani kwa mshukiwa ambaye alikamatwa na polisi na anasubiria kufunguliwa mashtaka.


Katika video ambazo zimesambaa mitandaoni, Mkurugenzi huyo kwa jina Baltasar Ebang Engonga mwenye umri wa miaka 54, amekuwa akishiriki mapenzi na wanawake wengi ikiwemo wake wa maafisa wakuu katika serikali ya Equitorial Guinea.


Katika kanda za video alizokuwa akirekodi, Engonga alionekana akifanya mapenzi na wake wakiwemo mke wa mkuu wa ulinzi wa rais wa nchi hiyo, mtoto wa mkuu wa jeshi la polisi, mke wa mwanasheria mkuu, binamu yake, mke wa mlinzi wake, mke wa mjomba wake ambaye ni mjamzito kati ya wake wa watu wengine mashuhuri nchini humo.


Kupitia ukurasa wa X, makamu wa rais wa nchi hiyo amesema kuwa serikali tayari imeanza kuwachukulia hatua maafisa ambao wameshiriki mapenzi katika ofisi za wizara mbali mbali kwa kuwaachisha kazi mara moja.


Makamu wa rais Nguema amesema kuwa serikali itawachukulia hatua kali dhidi ya visa hivyo, akiongeza kuwa ni ukiukaji wa wazi wa kanuni za maadili na sheria ya maadili ya umma.


ā€œMaadili na heshima ni mambo ya msingi katika utawala wetu na hatutaruhusu tabia ya kutowajibika ihatarishe imani ya umma.ā€  Alisema makamu huyo wa rais.


Aidha katika juhudi za kukabiliana na visa kama hivyo, makamu huyo wa rais amesema kuwa serikali itawekeza katika kuweka kamera za CCtv katika kila ofisi inayoomilikiwa na taasisi za serikali.


Makamu rais Teddy Nguema serikali imelazimika kuchukua hatua hiyo kuhakikisha kwamba sheria kwa maafisa wa umma inafuatwa ili kuondoa tabia hiyo mbovu.


Teodoro Obiang vile vile amesema kamwe serikali haitakubali kosa lolote linalodhalilisha uadilifu wa utawala wa Equitorial Guinea na wale wanaojihusisha na vitendo hivi watakabiliwa na hatua kali.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logoĀ© Radio Jambo 2024. All rights reserved