logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu 12 wauawa kwa kupigwa risasi Montenegro

Mtu mwenye silaha amewaua kwa risasi watu 12, wakiwemo watoto wawili, kusini mwa Montenegro.

image
na BBC NEWS

Kimataifa02 January 2025 - 16:00

Muhtasari


  • Shambulio la Jumatano lilitokea ndani ya mkahawa katika eneo la Cetinje kufuatia mabishano ya maneno, kulingana na serikali.


Mtu mwenye silaha amewaua kwa risasi watu 12, wakiwemo watoto wawili, kusini mwa Montenegro, polisi wamesema.

Shambulio la Jumatano lilitokea ndani ya mkahawa katika eneo la Cetinje kufuatia mabishano ya maneno, kulingana na serikali.

Serikali ya nchi hiyo imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kuanzia Alhamisi, huku Waziri Mkuu Milojko Spajic akisema ufyatuaji risasi "umechafua nchi yetu.”

Polisi walisema shambulio hilo lilianza pale mwanamume aliyeitwa Aleksandar Martinović, 45 - alipofyatua risasi katika mkahawa huo.

Aliwaua watu wa familia yake, watoto wawili wa mmiliki wa mgahawa huo - wenye umri wa miaka 10 na 13 - na pia mmiliki, kulingana na kamanda wa polisi wa Montenegro.

Mshambuliaji huyo kisha akaendelea kuua watu zaidi katika maeneo mengine.

Kulingana na polisi, mshukiwa alikuwa amekunywa pombe kupita kiasi kabla ya shambulio hilo kuanza.

Watu wanne walipelekwa hospitalini baada ya kujeruhiwa vibaya kwa risasi.

Mshambulizi huyo alikimbia lakini baadaye alijijeruhi vibaya baada ya kuzingirwa na polisi waliomtaka adondoshe silaha yake, polisi walisema.

Alifariki akiwa njiani kupelekwa hospitali.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved