logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ghana yazindua visa ya bila malipo kwa Waafrika wote

Wamiliki wote wa pasipoti wa Kiafrika sasa wanaweza kuzuru Ghana bila kuhitaji visa.

image
na BBC NEWS

Kimataifa04 January 2025 - 10:04

Muhtasari


  • Ghana sasa ni nchi ya tano barani Afrika kutoa hii kwa wasafiri kutoka bara zima.


Wamiliki wote wa pasipoti wa Kiafrika sasa wanaweza kuzuru Ghana bila kuhitaji visa, Rais anayemaliza muda wake Nana Akufo-Addo amesema.

Alitangaza mpango huo mwezi uliopita lakini katika hotuba yake ya mwisho ya hali ya taifa siku ya Ijumaa alisema kuwa sera hiyo ilianza kutekelezwa mwanzoni mwa mwaka.

Usafiri bila visa ndani ya bara kwa muda mrefu umekuwa hamu kwa wale wanaokuza maadili ya Uafrika na inaonekana kuwa muhimu kwa ushirikiano wa kiuchumi.

Ghana sasa ni nchi ya tano barani Afrika kutoa hii kwa wasafiri kutoka bara zima.

Nchi nyingine ni Rwanda, Ushelisheli, Gambia na Benin.

"Ninajivunia kuidhinisha safari bila viza kwenda Ghana kwa wamiliki wote wa pasipoti wa Kiafrika, kuanzia mwanzoni mwa mwaka huu," Akufo-Addo aliwaambia wabunge katika hotuba yake ya mwisho bungeni kabla ya kujiuzulu wiki ijayo baada ya miaka minane mamlakani.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved