logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Operesheni ya Marekani na Somalia yaua wanamgambo wa al-Shabab

Operesheni hiyo ilifanyika katika Kijiji cha Berhano, takriban kilomita 35 kutoka mji wa Kismayu.

image
na OTIENO TONNY

Kimataifa08 January 2025 - 11:53

Muhtasari


  • Vituo  vya magaidi viliharibiwa wakati wa operesheni hiyo, na hakuna raia aliyejeruhiwa .
  • Jeshi la Marekani Jumatatu lilithibitisha kuuawa kwa kiongozi mkuu wa al-Shabab Mohamed Mire katika shambulio la anga la Desemba 24.


  Wanamgambo wa Alshabab waliuawa katika operesheni iliyotekelezwa na wanajeshi wa nchi ya Somalia kwa ushirikiano na wanajeshi wa Marekani wa anga mnamo tarehe 5, Januari 2025.

Operesheni hiyo ilifanyika katika Kijiji cha Berhano, takriban kilomita 35 kutoka mji wa Kismayo. Vituo muhimu vya magaidi viliharibiwa wakati wa operesheni hiyo, na hakuna raia aliyejeruhiwa hii ni kutokana na ujumbe iliochapishwa kwenye mtandao ya X kupitia wizara ya habari, utamaduni na utalii nchini Somalia.

Jeshi la Marekani Jumatatu lilithibitisha kuuawa kwa kiongozi mkuu wa al-Shabab Mohamed Mire katika shambulio la anga la Desemba 24 karibu na mji wa Kunyo Barrow katika eneo la chini la Shabelle.

‘’Mnamo Desemba 24, kwa uratibu na ushirikiano  na serikali ya shirikisho la Somalia, Amri ya jeshi la Marekani barani Afrika  ilifanya shambulizi la anga la takriban kilomita 10 kusini magharibi mwa Quyno Barrow ambalo lilisababisha kifo cha kiongozi mkuu wa al-Shabaab, Mohamed Mire na mwanamgambo mwingine wa al-Shabaab,’’ Hii ni kutokana na mujibu wa U.S.Africa Command kupitia mtandao yao ya X.

Katika ujumbe yao amri ya jeshi la Marekani barani Afrika AFRICOM ilieleza kuwa Mire, anayejulikana pia kama Abu Abdirahman, aliwajibika kwa utawala wa kikanda wa al-Shabaab nchini Somalia kwa miaka 15 iliyopita. Mbali na kuwa mmoja wa wanachama waliokaa muda mrefu zaidi wa al-Shabaab, Mire aliwahi kuwa waziri wa mambo ya ndani na alichukua nafasi muhimu katika kufanya maamuzi ya kimkakati ya kundi hilo.

‘’Tutaendelea kutathmini matokeo ya operesheni hiyo na kutoa maelezo ya ziada kadri inavyofaa,” Alisema Jenerali wa jeshi la wanamaji la Marekani Michael Langley, kamanda wa AFRICOM, kulingana na taarifa hiyo.

AFRICOM ilisema haiwezi kufichua maelezo mahususi ya misheni hiyo, ikisema tu kwamba hakuna raia aliyejeruhiwa.

Al-Shabab, ambayo imekuwa ikipambana na serikali ya Somalia kwa zaidi ya miaka 15, inadhibiti maeneo makubwa kusini mwa Somalia na kutawala  eneo la kati la nchi hiyo na hata kushambulia nchi za jirani.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved