Chama cha wapiganiaji wa uhuru wa uchumi EFF cha Afrika Kusini kinachoongozwa na Julius Malema kimekubali kujiuzulu kwa wanachama wake wawili Yazini Tatyana na daktari Mbuyiseni Ndlozi kama wanachama wake katika uwakilishi kwenye bunge la kitaifa la nchi hiyo.
Julius Malema alikuwa kati ya wagombea wa urais wa Afrika Kusini katika uchaguzi uliofanyika mwaka jana ila alipoteza na baadaye kuchaguliwa tena kama kiongzoi wa chama cha EFF mwezi Agosti mwaka jana.
Kupitia taarifa kwa vyombo vya habari mapema Alhamisi asubuhi, cham cha EFF kimedhibitisha kupokea barua za kujiuzulu kwa waili hao na kimeridhia kuheshimu maombi yao ya kutaka kacha kuwa wawakilishi wa EFF kwenye bunge la Afrika Kusini.
Maombi ya kujiuzulu kwa Ndlozi na Tetyana yametwaja kuwa ya hiari kutoka kwa viongozi hao wawili.