logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu mashuhuri wamepoteza mali zao katika mlipuko wa moto wa Los Angeles

Mkasa wa moto katika eneo la Los Angeles umeathiri watu wengi hasa wale wa Hollywood

image
na OTIENO TONNY

Kimataifa10 January 2025 - 15:21

Muhtasari


  • Crystal na mkewe, Janice, walitoa taarifa Jumatano wakisema kuwa nyumba yao ya miaka 45 katika kitongoji cha Pacific Palisades ilikuwa imeharibiwa kutokana na moto huo.
  • Janga hilo ilianza Jumanne 7, Januari 2025.


Mkasa wa moto katika eneo la Los Angeles imeathiri watu wengi hasa wale wa jumuiya ya Hollywood, wakiwemo Billy Crystal, Mandy Moore, Jeff Bridges, Anna Faris na Ricki Lake miongoni mwa wengine wengi.

Mioto mikali huko Kusini mwa California imewalazimu wakazi zaidi ya 80,000  wa Los Angeles kuhama nyumba zao, wengi wao wameita eneo hilo nyumbani kwa miongo kadhaa wakiwemo baadhi ya nyota wakubwa wa Hollywood.

Janga hilo ilianza Jumanne 7, Januari 2025,  asubuhi katika eneo la Pacific Palisades , na moto uliofuata ulizuka katika jamii za karibu kama vile Eaton na Woodley.

Crystal na mkewe, Janice, walitoa taarifa Jumatano wakisema kuwa nyumba yao ya miaka 45 katika kitongoji cha Pacific Palisades ilikuwa imeharibiwa kutokana na moto huo.

‘’Janice nami tuliishi nyumbani kwetu tangu 1979. Tulilea watoto na wajukuu wetu hapa. Kila inchi ya nyumba yetu ilijaa upendo. Kumbukumbu nzuri ambazo haziwezi kuondolewa, hakika tumeumia moyoni lakini kwa upendo wa watoto wetu na marafiki tutapitia haya,” Familia ya Crystal iliandika kwenye taarifa hiyo.

Mwigizaji na mtangazaji wa zamani wa kipindi cha mazungumzo kwa jina Lake alichapisha  kwenye ukurasa wake wa Instagram Jumatano kwamba alipoteza "nyumba ya ndoto" kwenye moto huo, akamaliza kuandika kuwa, "Yote yamepita."

‘’Ilikuwa mbingu yetu hapa duniani. Mahali tulipopanga kuzeeka pamoja.hatukuwahi kuchukua nafasi yetu ya kimbingu kwa upuuzi unaongalia Malibu yetu mpendwa kwa urahisi, hata kwa sekunde moja,’’ Aliandika haya Lake.

Paris Hilton aligundua kuwa nyumba yake ya Malibu ilipotea wakati akiitazama ikiteketea kwenye televisheni  ya moja kwa moja. Akiandika katika ukurasa wake wa Instagram alisema kuwa picha hiyo ni kitu hakuna mtu anayepaswa kuona au kupitia.

Mpishi mashuhuri Sandra Lee pia alisema alipoteza nyumba yake kutokana na janga hilo la moto. Alikuwa alisema kuwa alisikitika na vitu zake za thamani zilizoungua katika nyumba yake.

“Nililia usiku kucha na kuwaza kuhusu kila chumba, chumba cha kulala na chumba cha kukula. Ilikuwa kamilifu na sasa ni jivu tu, Tafadhali waweke jumuiya yetu, wazima moto na waitikiaji wa kwanza katika maombi yako. Hii haijaisha na hata haikaribii kuisha bado." Aliandika Lee kwenye ukurasa wa Instagram.

Watu wengi mashuhuri wa hollyhood wanapitia wakati mgumu baada ya kugundua kwamba kitongoji chao cha matajiri cha Los Angeles kilibadilika kuwa majivu na vifusi wakati moto ulizuka Califonia na kusambaa palisades kote.

Idadi ya waliofariki kwenye moto huo wa kihistoria sasa imefikia 10, huku wazima moto mashujaa bado wanapambana na hali mbaya kwenye msatri wa mbele wa angalau moto tano tofauti.

Nyumba za Paris Hilton, Anthony Hopkins, Tina Knowles, John Goodman, Candy Spelling, Milo Ventimiglia, na Miles Teller ni miongoni mwa zilizoharibiwa, huku makumi ya nyota wengine sasa wanakabiliwa na kusubiri kwa wasiwasi pamoja na majirani zao ili kujua kama kuna baadhi ya vitu zao zilizookolewa.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved