logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Waasi wawaua wanajeshi 13 wa kigeni wa kulinda amani DR Congo

Umoja wa Mataifa unawaondoa wafanyakazi wote wasio wa lazima kutoka Goma.

image
na Samuel Mainajournalist

Kimataifa26 January 2025 - 13:05

Muhtasari


  • Wanajeshi 13 wanaohudumu na vikosi vya kulinda amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wameuawa katika makabiliano na waasi wa kundi la M23.


Wanajeshi 13 wanaohudumu na vikosi vya kulinda amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wameuawa katika makabiliano na waasi wa kundi la M23.

Jeshi la Afrika Kusini lilisema wanajeshi wake tisa wameuawa wakisaidia kuwarudisha nyuma waasi katika mji wa Goma, mashariki mwa DR Congo, huku raia watatu wa Malawi na Uruguay pia wakiuawa.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alisema amezungumza na viongozi wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na Rwanda huku kukiwa na wito wa kimataifa wa kutaka ghasia hizo zisitishwe.

Umoja wa Mataifa unawaondoa wafanyakazi wote wasio wa lazima kutoka Goma - jiji lenye zaidi ya watu milioni moja - wakati mapigano yanapozidi.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved