Wanajeshi 13 wanaohudumu na vikosi vya kulinda amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wameuawa katika makabiliano na waasi wa kundi la M23.
Jeshi la Afrika Kusini lilisema wanajeshi wake tisa wameuawa wakisaidia kuwarudisha nyuma waasi katika mji wa Goma, mashariki mwa DR Congo, huku raia watatu wa Malawi na Uruguay pia wakiuawa.
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alisema amezungumza na viongozi wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na Rwanda huku kukiwa na wito wa kimataifa wa kutaka ghasia hizo zisitishwe.
Umoja wa Mataifa unawaondoa wafanyakazi wote wasio wa lazima kutoka Goma - jiji lenye zaidi ya watu milioni moja - wakati mapigano yanapozidi.