logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sonko amlipia mwanamume aliyeiba Naivas faini ya Sh100,000

Chivondo ndiye alikuwa gumzo nchini kufuatia uamuzi wa mahakama.

image
na Radio Jambo

Makala13 April 2022 - 19:53

Muhtasari


  • Mahakama ilimtoza Alvin Chivondo faini ya Sh100,000 au kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kuiba bidhaa za thamani ya Sh3,165
  • Bidhaa hizo ni pamoja na mchele kilo 5, mafuta ya kula lita 5 na sukari kilo 2
Aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko

Aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko amelipa faini aliyotozwa mwanamume aliyepatikana na hatia ya wizi wa duka kutoka kwa duka kuu la Naivas.

Mahakama ilimtoza Alvin Chivondo faini ya Sh100,000 au kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kuiba bidhaa za thamani ya Sh3,165.

Bidhaa hizo ni pamoja na mchele kilo 5, mafuta ya kula lita 5 na sukari kilo 2.

Sonko alisema kwamba alifanya uamuzi huo kama njia yake ya kawaida ya kuwafikia watu wenye matatizo.

"Wakenya wengi wanaishi katika maisha duni kutokana na janga la COVID-19, wengi watasema kwamba ni PR lakini napenda kusaidia watu, hilo limekuwa shauku yangu tangu nikiwa shule ya upili huko Kwale boys," Sonko alisema.

Aliongeza kuwa:

"Pia nimeahidi kumpa hisa ya chakula cha mwezi mmoja pamoja na kumpa kazi pia."

Sonko pia amewataka wapinzani kutoingiza siasa katika kesi ya Alvin, na kwamba hakulipa faini yake kutafuta hatua zozote za kisiasa.

Chivondo ndiye alikuwa gumzo nchini kufuatia uamuzi wa mahakama.

Kiongozi wa ODM Raila Odinga alitoa wito wa kuachiliwa bila masharti kwa mshukiwa.

Katika tweet Jumatano, Raila alidai Chivondo aachiliwe bila masharti.

"Alvin Linus Chivondo aachiliwe bila masharti! Wahalifu sasa wanapata ahueni ya kufanya kampeni kwa uhuru, huku wahalifu wadogo wakifungwa jela," Raila alisema.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved