Mahakama yatupilia mbali kesi ya kubadilisha tarehe ya uchaguzi

Muhtasari

• Jaji Anthony Mrima alisema Uchaguzi Mkuu ufanyike kwa wakati mmoja na kwamba si jambo la kujadiliwa. 

• Hoja hii ilitupiliwa mbali na mahakama kwa vile tume sasa ina Mkurugenzi Mtendaji.

• Hii ina maana kwamba Uchaguzi Mkuu ujao unatarajiwa kufanyika tarehe 9 Agosti 2022.

Mahakama Kuu imekataa kuahirisha Uchaguzi Mkuu ujao uliopangwa kufanyika Agosti 9, ikisema tarehe hiyo ni ya kikatiba. 

Jaji Anthony Mrima alisema Uchaguzi Mkuu ufanyike kwa wakati mmoja na kwamba si jambo la kujadiliwa. 

"Agosti 9 kikatiba ni Jumanne ya pili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka wa tano. Katiba iko wazi kuhusu tarehe ya uchaguzi. Katiba haiwezi kujipindua," alisema. 

Kesi hiyo iliwasilishwa na aliyekuwa Seneta maalum Paul Njoroge. Njoroge alikuwa amedai kwamba tume ya uchaguzi na mipaka IEBC haikuundwa ipasavyo wakati ikitangaza tarehe ya Uchaguzi Mkuu ujao. 

Hoja hii ilitupiliwa mbali na mahakama kwa vile tume sasa ina Mkurugenzi Mtendaji. Pia aliteta kuwa muhula wa Rais Uhuru Kenyatta na Naibu Naibu Rais William Ruto ungeisha mnamo Novemba kwa sababu uchaguzi uliopita ulifanyika Oktoba 26, 2017. 

Hata hivyo, Katiba inataka Uchaguzi Mkuu ufanyike Jumanne ya pili ya Agosti kila mwaka wa tano.

Hii ina maana kwamba Uchaguzi Mkuu ujao unatarajiwa kufanyika tarehe 9 Agosti 2022.