logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanaume ashtakiwa kwa kupiga na kujeruhi wanawe mapacha wa miezi 6

Aliachiliwa kwa dhamana ya Sh500,000 bila chaguo la dhamana ya pesa taslimu. Kesi hiyo itatajwa Julai 26, 2022.

image
na Radio Jambo

Habari14 July 2022 - 07:04

Muhtasari


• Mapacha hao wamelazwa katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta.

Fredrick Okello katika mahakama ya Kibera ambapo alishtakiwa kwa madhara makubwa

Mwanaume mmoja alifikishwa katika mahakama ya Kibera kwa kosa la kuwapiga na kuwajeruhi vibaya watoto wake mapacha wa miezi 6.

Mwanaume huyo aliyetambulika kwa jina Fredrick Okello, 24, ilisemekana aliachiwa watoto na mama yao ambaye aliondoka kwenda kwa Jirani na aliporudi akapata pacha wa kiue analia kwa maumivu makubwa.

Mama watoto alipojaribu kuuliza tatizo, pia Okello alimpokeza kichapo na hata kumzuia ndani ili asiwapeleke watoto hospitalini.

Kitendo hicho kilitokea mnamo tarehe 6 Julai katika makaazi yao eneo la mtaa wa mabanda wa Raila na mahakama ilijulishwa kwamba mapacha hao bado wamelazwa katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta katika chumba cha wagonjwa mahututi.

Mwendesha mashtaka Nancy Kerubo aliiambia mahakama kwamba mmoja wa mapacha hao alivunjika mguu na hivyo kuitaka mahakama kumzuilia mshtakiwa kwa siku nyingine zaidi bil kumpa dhamana.

Mshtakiwa alikana mashtaka mbele ya Hakimu Mkuu Mwandamizi Esther Bhoke katika Mahakama ya Kibera. Aliachiliwa kwa dhamana ya Sh500,000 bila chaguo la dhamana ya pesa taslimu. Kesi hiyo itatajwa Julai 26, 2022.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved