logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kesi ya mauaji ya mbunge Barasa yahamishiwa mahakama kuu ya Bungoma

Hakuna pande yoyote iliyopinga uhamishaji wa faili hiyo.

image
na

Makala14 November 2022 - 08:18

Muhtasari


•Mahakama kuu ya Kakamega imeagiza faili ya kesi hiyo kuwekwa mbele ya jaji msimamizi wa mahakama kuu ya Bungoma.

•Katika kesi hiyo, Barasa ameshtakiwa kwa mauaji ya Brian Olunga, msaidizi wa mpinzani wake Brian Khaemba.

Kesi ya mauaji ya mbunge wa Kimilili Didmus Barasa imehamishiwa katika mahakama kuu ya Bungoma.

Mahakama kuu ya Kakamega imeagiza faili ya kesi hiyo kuwekwa mbele ya jaji msimamizi wa mahakama kuu ya Bungoma.

Mahakama ilisema kwa kuwa kisa hicho kilifanyika Bungoma, ilikuwa sawa kwa kesi hiyo kufanyika huko na wala si Kakamega alikofunguliwa mashtaka.

Hakuna pande yoyote iliyopinga uhamishaji wa faili hiyo.

Afisa anayeongoza uchunguzi pia ameagizwa kuwapa mawakili wa mwathiriwa taarifa zote za mashahidi na ushahidi mwingine wa maandishi.

Kesi hiyo itatajwa Novemba 24 mbele ya hakimu mfawidhi kwa maelekezo zaidi kuhusu jinsi itakavyoendelea.

Katika kesi hiyo, Barasa ameshtakiwa kwa mauaji ya Brian Olunga, msaidizi wa mpinzani wake Brian Khaemba.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved