logo

NOW ON AIR

Listen in Live

James Ndichu apatikana na hatia ya kuwapa wateja dawa kinyume cha sheria kwa malengo ya kuwanajisi

Katika utetezi wake, Mugo alimtaka hakimu kumwachilia huru kwa kukosa ushahidi.

image
na Radio Jambo

Habari17 November 2022 - 13:12

Muhtasari


  • Katika utetezi wake, Mugo alimtaka hakimu kumwachilia huru kwa kukosa ushahidi
  • Aliteta kuwa hakuwahi kukutana na mwanamke aliyedaiwa kumbaka katika kliniki yake

Daktari James Mugo Ndichu, almaarufu Wairimu, amepatikana na hatia ya kuwapa wagonjwa dawa kinyume cha sheria katika kliniki yake mwaka wa 2015.

Hakimu mkuu wa mahakama ya Milimani Wendy Micheni mnamo Alhamisi aligundua kuwa Mugo, ambaye alishtakiwa kwa makosa 12 alikuwa na hatia ya makosa 10.

Mahakama ilimtia hatiani kwa kuendesha kituo cha matibabu kinyume cha sheria, kuwapa wagonjwa wake dawa kinyume cha sheria miongoni mwa wengine.

Wendy alisema upande wa mashtaka ulithibitisha kesi yake bila shaka dhidi yake.

Hata hivyo, ameachiwa huru kwa tuhuma za kumbaka mgonjwa wake na kuwaajiri wanafunzi wawili kinyume cha sheria kufanya naye kazi katika zahanati yake kutokana na kukosekana kwa ushahidi.

Katika utetezi wake, Mugo alimtaka hakimu kumwachilia huru kwa kukosa ushahidi.

Aliteta kuwa hakuwahi kukutana na mwanamke aliyedaiwa kumbaka katika kliniki yake.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved