logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Chifu mkuu mstaafu ashtakiwa kwa kumnajisi msichana wa shule

Chifu huyo alifika mbele ya hakimu mkazi mkuu Christine Menya na kukana mashtaka mawili ya unajisi.

image
na

Habari17 January 2023 - 13:29

Muhtasari


  • Sang ambaye pia ni afisa mstaafu wa GSU na ana umri wa miaka 68 aliachiliwa kwa bondi ya sh 200,000 na udhamini sawa na huo

Chifu mkuu mstaafu katika mji wa Eldoret William Sang ameshtakiwa kwa kumnajisi msichana wa shule siku ya Boxing day Desemba mwaka jana.

Chifu huyo alifika mbele ya hakimu mkazi mkuu Christine Menya na kukana mashtaka mawili ya unajisi.

Inadaiwa alitenda kosa hilo katika eneo la Kaptagat Kerio Valley ndani ya Kaunti ya Elgeyo Marakwet.

Sang ambaye pia ni afisa mstaafu wa GSU na ana umri wa miaka 68 aliachiliwa kwa bondi ya sh 200,000 na udhamini sawa na huo.

Menya aliamuru kesi hiyo itajwe Februari 6 kwa mkutano wa awali wa kesi hiyo.

Wakati huo huo hakimu alieleza kushangazwa na ongezeko la kesi ambapo vijana wengi wamefunguliwa mashtaka ya kutishia kuwaua mama zao mkoani humo.

Aliuliza upande wa mashtaka kujua kwa nini kumekuwa na ongezeko la kesi kama hizo.

Alitoa maoni hayo baada ya zaidi ya vijana 10 kushtakiwa tofauti kwa makosa ya kutishia kuwaua mama zao.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved