logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jamaa akiri kosa la kukata miti katika Mbuga ya Kitaifa ya Nairobi

Aliiambia mahakama kuwa alijuta sana, lakini akadai yeye ni maskini na ni mtu mwenye familia.

image
na

Habari19 January 2023 - 03:47

Muhtasari


•Samuel Gicheru alikiri mashtaka mbele ya hakimu mkuu mwandamizi wa Kibera Esther Boke siku ya Jumatano.

•Aliiambia mahakama kuwa alijuta sana, lakini akadai yeye ni maskini na ni mtu mwenye familia.

Mwanamume mmoja amekiri kosa la kuiba miti katika Hifadhi ya Kitaifa ya Nairobi.

Samuel Gicheru alikiri mashtaka mbele ya hakimu mkuu mwandamizi wa Kibera Esther Boke siku ya Jumatano.

Gicheru alishtakiwa kwa kukata miti ya Acacia mnamo Januari 14 kando ya barabara ya Southern Bypass.

Kulingana na upande wa mashtaka, Gicheru alikamatwa na maafisa ambao walikuwa wakishika doria.

 "Maafisa hao walimwona akikata miti na akaamriwa kukomesha alichokuwa akifanya kwani ilikuwa kinyume cha sheria katika eneo lililohifadhiwa," mahakama ilisikiza.

Aliiambia mahakama kuwa alijuta sana, lakini akadai yeye ni maskini na ni mtu mwenye familia.

Gicheru alitozwa faini ya Sh10,000 au kutumikia kifungo cha miezi sita jela.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved