logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Eldoret: Mshukiwa amuomba hakimu kumnunulia ugali kabla ya kumsomea mashtaka

Olindo aliomba pia kuachiliwa kwac dhamana ya 2k ili arudi kwa mke wake asichukuliwe.

image
na Radio Jambo

Habari14 March 2023 - 11:50

Muhtasari


• Olindo pia alimtaka hakimu kumpa dhamana ya elfu 2 kwani angeendelea kuzuiliwa wahuni wangemchukua mke wake.

Mahakama

Mlinzi aliyetiwa mbaroni kwa tuhuma za kumshambulia mtu alizua kicheko katika mahakama ya Eldoret aliposema kwamba hangeweza kufuatilia mashtaka dhidi yake pasi na kupatiwa ugali.

Japhet Olindo alifikishwa mahakamani na kabla ya kuanza kusomewa mashtaka dhidi yake, alimuomba hakimu Keynes Odhiambo kumnunulia ugali mwanzo kabla ya shughuli yoyote kung’oa nanga.

Mshukiwa huyo alidai kwamba alikuwa katika hali mbaya karibu kuzimia kwa kile alitaja kwamba hakuwa amekula ugali – chakula chake pendwa tangu kuwekwa kizuizini.

Alimuomba hakimu kumfanyia mpango wa chakula hicho kwani bila hivyo hangeweza kuwa na umakini wa kufuatilia kesi dhidi yake mahakamani.

Hata hivyo, hakimu alimpa hakikisho la kuvumilia asomewe mashtaka na baadae amnunulie chakula hicho.

Kando na ombi la chakula, bwana Olindo pia aliomba hakimu kumpa adhabu ya chini na kumuachilia kwa dhamana ya elfu 2 kwa kile alisema kwamab angekaa jela kwa muda mrefu Zaidi, wahuni wangevamia boma lake nyumbani na kumnyakua mke wake.

Alikanusha mashtaka dhidi yake ya kuwashambulia watu watatu mnamo Machi 10 na kuachiwa kwa dhamana ya elfu 2 akisubiriwa kesi yake kutajwa tena mnamo Machi 16.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved