logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kasarani: Mrembo amwekea mwanamume dawa kwenye pombe, kisha kumuibia Ksh 849K

Simu yake yenye thamani ya laki mbili na nusu iliibiwa pia.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri31 March 2023 - 09:24

Muhtasari


• Bw Sang alikuwa akifurahia vinywaji kwenye mkahawa mmoja na marafiki zake alipojumuika na mwanamke asiyemfahamu.

• Alipata taarifa za benki na kugundua kuwa Sh849,000 zilikuwa zimetolewa kutoka kwa akaunti yake ya benki. Pesa hizo zilitumwa kwa nambari tofauti za simu kupitia M-Pesa.

Mwanamke amwekea 'mchele' mwanamume kwenye baa kisha kumuibia 849k

Mwanamke mmoja anayedaiwa kumwekea dawa mtu katika baa mmoja huko Kasarani, Nairobi kabla ya kutoa Sh849,000 kutoka kwa akaunti zake tatu za benki baada ya kuiba simu yake alishtakiwa kwa kosa hilo.

Kwa mujibu wa ripoti zilizopo katika jarida la Nation, mwanamke huyo alimfanyia Fredrick Sang madhambi hayo Machi 12 kabla ya kumuibia pesa hizo pamoja na simu yenye thamani ya laki mbili na nusu.

Bw Sang alikuwa akifurahia vinywaji kwenye mkahawa mmoja na marafiki zake alipojumuika na mwanamke asiyemfahamu.

Baada ya kunywa kwa muda, Bw Sang aliondoka kwenye mkahawa huo na mwanamke huyo baada ya kumwomba ampeleke katika makazi yake katika mtaa wa Thome, Kasarani.

Mlalamishi aliamka siku iliyofuata na kujipata peke yake ndani ya gari lake lililoegeshwa katika kituo cha mafuta katika mtaa wa Thome. Mwanamke huyo alikuwa ametoweka, Nation waliripoti.

Simu zake mbili, kitambulisho cha taifa na kadi mbili za ATM pia hazikuwepo. Akaendelea na kazi. Wenzake walimjulisha kuwa simu zake zilikuwa zikiita bila kupokelewa.

Alipata taarifa za benki na kugundua kuwa Sh849,000 zilikuwa zimetolewa kutoka kwa akaunti yake ya benki. Pesa hizo zilitumwa kwa nambari tofauti za simu kupitia M-Pesa.

Baadaye Bw Sang alitafuta matibabu katika kliniki ambapo madaktari walimwambia kwamba vinywaji vyake vilikuwa vimewekwa dawa kwa kiwango kikubwa.

Baadaye aliripoti kisa hicho katika kituo cha Polisi cha Kasarani na idara ya Upelelezi wa Jinai ilichukua jukumu la uchunguzi.

Mwanamke ambaye alikuwa pamoja naye alifuatiliwa baadaye, akakamatwa na kushtakiwa kwa mashtaka yaleyale. Aliachiliwa kwa bondi ya Shilingi milioni 1.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved