logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mahakama yaahirisha kutoa uamuzi katika kesi ya mauaji dhidi ya Jowie na Maribe

Wawili hao wanashtakiwa kwa mauaji ya mfanyabiashara Monica Kimani 2018.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri06 October 2023 - 08:37

Muhtasari


• Jaji wa Mahakama Kuu Grace Nzioka alipaswa kutoa uamuzi huo leo, baada ya kumalizika kwa kesi hiyo mwezi Julai, lakini imeripotiwa kwamba hakuweza kufanya hivyo kutokana na ugonjwa.

Jacque Maribe na Jowie Irungu mahakamani

Mahakama kuu jijini Nairobi imeahirisha uamuzi wa kesi ya mauaji dhidi ya Joshua Irungu almaarufu Jowie na aliyekuwa mtangazaji wa televisheni Jacqueline Maribe hadi Desemba 15, 2023.

Jaji wa Mahakama Kuu Grace Nzioka alipaswa kutoa uamuzi huo leo, baada ya kumalizika kwa kesi hiyo mwezi Julai, lakini imeripotiwa kwamba hakuweza kufanya hivyo kutokana na ugonjwa.

Wapenzi hao wawili wa zamani wanashtakiwa kwa mauaji ya mfanyabiashara Monica Kimani ambaye alipatikana amefariki kwa kukatwa koromeo nyumbani kwake Nairobi Septemba 2018.

Joseph Irungu akiwa ameshika bunduki ya kivita akiwa na jeraha la risasi. Mfanyabiashara aliyeuawa Monicah Kimani

Kesi hiyo ilipomalizika mwezi Julai, upande wa utetezi uliwasilisha hoja zao za mwisho ambapo Irungu na Maribe, kupitia kwa mawakili wao, waliiomba mahakama iwaachilie huru.

Waliteta kuwa upande wa mashtaka ulikosa kuthibitisha bila shaka kuwa wana hatia ya kumuua Monica ambaye alipatikana ameuawa kikatili nyumbani kwake huko Lamuria Gardens.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved