logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Washukiwa 4 wa ubakaji wafungwa jela miaka 15

Mahakama ilibaini kuwa ushahidi uliowasilishwa mbele yake uliwa mzito wa kuwahukumu washukiwa

image
na Brandon Asiema

Mahakama05 November 2024 - 14:30

Muhtasari


  • Washukiwa walitekeleza kitendo hicho Septemba 23 mwaka wa 2023 katika kijiji cha Sirwet, Baringo kusini

caption

Mahakama ya Kabarnet katika kaunti ya Baringo imewafunga washukiwa wanne wa ubakaji miaka 15 kila mmoja baada ya kupatikana na hatia ya ubakaji wa genge.


Kesi hiyo iliyosikilizwa mbele ya hakimu Edwin Mulochi ilisema kuwa ushahidi uliowasilishwa na mashahidi ulikuwa wa kutosha na wenye uzito mkubwa dhidi ya washukiwa.


Hakimu Edwin Mulochi aliwapata washukiwa hao kwa majina Benard Kiprop, Jackson Cheruiyot, Kurgat Chebotibin na Benson Cheruiyot na hatia kinyume na kifungu cha 10 cha sheria ya vitendo vya ukatili wa kijinsia.


Mashahidi waliowasilishwa na Rebecca Bartilol walitoa ushahidi ambao mahakama ilitaja kuwa ulionyesha hatia kwa washtakiwa bila shaka yoyote na kupita viwangovya kisheria vinavyohitajika kwa ajili ya kutiwa hatiani.


Wafungwa hao walipatikana na hatia ya kutekeleza ubakaji huo mnamo Septemba tarehe 24 mwaka wa 2023mwendo wa saa moja jioni katika kijiji cha Sirwet, kaunti ndogo ya Baringo Kusini.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved