logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jamaa Aliyekamatwa Na Vipande Vya Mwili Wa Mkewe Nairobi Azuiliwa Kwa Siku 21

Hakimu Gilbert Shikwe aliruhusu ombi lililotolewa na maafisa wa DCI katika Kaunti Ndogo ya Starehe ili kuwawezesha kupata viungo vingine vya mwili ambavyo bado havijapatikana.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Mahakama22 January 2025 - 16:19

Muhtasari


  • Polisi walisema pia wanahitaji kurekodi taarifa za mashahidi wakuu wa upande wa mashtaka na kufanya vipimo vya DNA ili kufahamu umri na utambulisho halisi wa marehemu.
  • Pia inahitajika wakati wa uchunguzi ni tathmini ya kiakili ambayo itafanywa kwa mtuhumiwa.



MAHAKAMA ya hakimu mkazi imeruhusu ombi la polisi kumzuilia mwanamume anayedaiwa kupatikana na sehemu za mwili za mkewe zilizokuwa zimekatwa Huruma kwa siku 21 kusubiri uchunguzi zaidi.


Hakimu wa mahakama ya Milimani Gilbert Shikwe aliruhusu ombi lililotolewa na maafisa wa DCI katika Kaunti Ndogo ya Starehe ili kuwawezesha kupata viungo vingine vya mwili ambavyo bado havijapatikana.


Mahakama ilisikia kwamba iwapo John Kyama Wambua ataachiliwa, huenda akaingilia uchunguzi huo kwani bado hawajapata silaha nyingine ya mauaji ambayo polisi wanashuku kuwa 'panga'.


Polisi walisema pia wanahitaji kurekodi taarifa za mashahidi wakuu wa upande wa mashtaka na kufanya vipimo vya DNA ili kufahamu umri na utambulisho halisi wa marehemu.


Pia inahitajika wakati wa uchunguzi ni tathmini ya kiakili ambayo itafanywa kwa mtuhumiwa.


Kulingana na hati ya kiapo iliyowasilishwa kortini, maafisa wa polisi walio katika kituo cha polisi cha Huruma wakiwa doria walimwona John akiwa amebeba begi kwenye begi lake.


"Alionekana mwenye mashaka," inasomeka sehemu ya hati ya kiapo.


Walimsimamisha na kuendelea na upekuzi kwenye begi na kugundua sehemu za mwili wa binadamu (sehemu ya kifua) zikiwa zimefichwa kwenye shehena ya saruji ya nailoni.


"Baada ya kuhojiwa, alituongoza hadi nyumbani kwake ambapo sehemu zingine za mwili zilipatikana," inasomeka hati ya kiapo.


Inaendelea kusema kuwa John anadaiwa kukiri kuwa ni wa mkewe-Joy Munani (marehemu).


Wakati akihojiwa, John alidaiwa kuwaambia maafisa hao kwamba alimkuta Joy akiwa na mwanamume mwingine, ugomvi ukazuka na hatimaye "kuukatakata mwili wake ili kuutupa"


Awali, polisi walisema mkono wa kushoto wa mwanamke huyo, kiuno na sehemu ya nyonga na paja moja la juu havikuwepo.


Mkuu wa polisi anayemaliza muda wake Adamson Bungei alisema nia ya mauaji hayo bado haijajulikana.


Polisi walisema kuwa familia ya marehemu ilitafutwa na watasaidia katika uchunguzi.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved