logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Collabo kati ya Diamond na Wiz Khalifa itabadilisha muziki wa Afrika Mashariki?

Ana sifa za kupata wataamaji  bilioni kwenye YouTube kwenye wimbo wake wa See You Again.

image
na Radio Jambo

Burudani07 July 2021 - 11:19

Muhtasari


  • Collabo kati ya Diamond na Wiz Khalifa itabadilisha muziki wa Afrika Mashariki?
Diamond Platnumz na Wiz Khalifa

Msanii nyota wa bongo Tanzania Diamond Platinumz ndiye msanii wa muziki aliyefanikiwa zaidi kutoka Afrika Mashariki na Kati.

Msanii uyo anafahamika sana kupitia kwenye bidii ya kazi yake na jinsi amekuwa akiwashirikisha wasanii tofauti katika muziki wake.

Njia yake ya muziki inaonekana kuwa ya kirafiki kwani amejihusisha na marafiki na familia yake kwa pamoja.

Muziki wake umeweza kuvutia kizazi cha wazee na kizazi kipya.Kweli utashangaa kupata mtoto wa miaka mitano akiimba wimbo wa Diamond barani Afrika.

Kimataifa, Diamond ameunda mtandao mkubwa wa wasanii na wapenzi wa muziki wake huku akitafuta kutambuliwa katika kiwango cha ulimwengu.

Diamond ameteuliwa na kutuzwa tuzo tofauti za muziki, licha ya changamoto za muziki msanii huyo hajaweza kufa moyo amezidi kutia bidii katika kazi yake ya usanii.

Ingawa amefanya ushirikiano na wasanii wa Amerika kama Ripiki Rick Ross, wasanii wa RNB Ne-Yo na Omarion, naamini ushirikiano wake na msanii wa nyimbo za hiphop wa Amerika Wiz Khalifa utakuwa mzuri na utabadilisha muziki wa Afrika mashariki.

Wiz Khalifa ametengeneza muziki bora kabisa kuwahi kusikika katika historia ya muziki wa hip hop ulimwenguni kote.

Ana sifa za kupata wataamaji  bilioni kwenye YouTube kwenye wimbo wake wa See You Again.

Ushirikiano wao ungeweza kuona Diamond Platinumz akpata watazamaji wa kiwango cha bilioni wakati wowote kwani Afrika anasikilizwa vizuri.

Swali kuu ni je collabo kati ya wasanii hao wawili itaweza au haitaweza, na je itabadili muziki wa Afrika Mashariki?

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved