Hizi hapa sababu kwa nini wanaume hukasirika sana baada ya kudanganywa kwenye uhusiano

Muhtasari
  • Hizi hapa sababu kwanini wanaume hukasirika sana baada ya kudanganywa kwenye uhusiano
  • Je umewahi jiuliza kwanini wanaume wengi, wakidanganywa au wake au mpenzi akienda nje ya uhusiano wa kimapenzi huwa wanakasirika kupita kiasi?

Je umewahi jiuliza kwanini wanaume wengi, wakidanganywa au wake au mpenzi akienda nje ya uhusiano wa kimapenzi huwa wanakasirika kupita kiasi?

Kauli ambayo imekuwa ikizunguka kwa suala la kudanganya kwa muda mrefu zaidi ni kwamba wanaume hudanganya zaidi kuliko wanawake, lakini wanaumia zaidi na wamefadhaika na hukasirika wanapogundua kuwa ' wamedanganywa.

Kauli hiyo inatuona tunaamini kwamba wanawake kwa namna fulani 'wanatarajia' kudanganywa kwa sababu 'wanaume wote hudanganya' na 'wanaume watakuwa wanaume siku zote.'

Kwa hivyo wacha tuzungumze juu ya sababu kwanini hii iko hivi.

Kwa nini inawasumbua wanaume sana wakati mwanamke anawadanganya, na kwa nini wanaume wengi huona udanganyifu hauwezi kusamehewa kabisa ikilinganishwa na wanawake?

1.Hawaoni kuwa wanaweza kudanganywa

Baadhi ya wanaume wamejiamini sana na kukiri kwamba hawawezi danganywa na wake zao au wapenzi wako.

Kwa kweli wengi huwa hawaoni hayo yakija maishani mwao, ndio maana hukasirika sana wakidanganywa.

2.Wamekuwa waaminifu kwa muda mrefu

Kuna wanaume ambao hawana tamaa na kukaa na mwanamke mmoja maishani mwao, lakini mwanamke akiwadanganya wanaumia na kuksirika sana maanake wamekuwa waaminifu katika uhusiano wao.

3.Wanajua kuwa kudanganya, kwa wanawake, ni kwa sababu za kihemko tu.

Wakati wanawake wanadanganya, ni kwa sababu za kihemko. Wanawake hawadanganyi kwa sababu za kimaumbile, na kwa sehemu kubwa sio kwa kuridhika kijinsia.

Imesemekana kwamba hitaji la kuziba pengo la kihemko, kuziba utupu wa kihemko ndio huongoza wanawake katika maswala.

4.Wanahisi udanganyifu ni wa wanaume pekee

Wengi wamejiamini kuwa wanaweza wadanganya wake zao na wasijue, lakini mwanamke ni nani atajua na kisha ataamua kulipiza kisasi hapo ndipo utatatambua kwamba kudanganya sio kwa wanaume tu bali kuna wataalamu wa wanawake ambao wanajua kudanganya.