logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Haya hapa mambo ambayo hukuyafahamu kuhusu Caroline Kangogo

Kangogo aligonga vichwa vya habari baada ya kumuua polisi mwenzake,katika hali isiyojulikana.

image
na Radio Jambo

Burudani16 July 2021 - 10:25

Muhtasari


  • Haya hapa mambo ambayo hukuyafahamu kuhusu Caroline Kangogo

Baada ya taarifa kuenea kwamba afisa mtoro Caroline Kangogo amefariki dunia, maswali mengi yameibuka miongoni mwa Wakenya.

Kangogo alipatikana ameaga dunia Ijumaa, Julai 16 nyumbani kwao Elgeyo Marakwet baada ya kutoweka tangu Julai 5.

Baada ya kutangazwa kwa kifo chake, Wakenya walifurika mitandaoni kutoa maoni yao kuhusiana na hisia zao.

Kangogo aligonga vichwa vya habari baada ya kumuua polisi mwenzake,katika hali isiyojulikana.

Haya hapa mambo ambayo hukujua kuhusu Caroline Kangogo;

Caroline amezaliwa Elgeyo Marakwet.

Koplo Kangogo alikuwa akihusishwa na mauaji mawili, alimpiga risasi polisi John Ogweno na mwanamume aliyefahamika kama Peter Njiiru.

Alisafiri kutoka Nakuru kwenda Thika kutekeleza mauaji ya pili.

Alikuwa na umri wa miaka 34.

Caroline alikuwa mama wa watoto wawili.

Alianza kufanya kazi katika kituo cha Polisi cha Nakuru mnamo 2015 hadi kifo chake.

Alijiunga na jeshi la polisi mnamo 5/8/2008.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved