logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu maarufu ambao walifunguka juu ya uhusiano wao wa kimapenzi 2021

Tumeona watu mashuhuri wakituhumiwa kujihusisha na mambo haramu,

image
na Radio Jambo

Yanayojiri03 September 2021 - 20:46

Muhtasari


  • Tangu mwaka uanze, kuna mambo mengi ambayo yametokea katika mitandao ya kijamii
  • Tumeona watu mashuhuri wakituhumiwa kujihusisha na mambo haramu, wengine wakianza uhusiano mpya

Tangu mwaka uanze, kuna mambo mengi ambayo yametokea katika mitandao ya kijamii.

Tumeona watu mashuhuri wakituhumiwa kujihusisha na mambo haramu, wengine wakianza uhusiano mpya, wakati wengine kama mwanamuziki wa Tanzania Harmonize akitupwa na wapenzi wao.

Katika makala haya , tutaangalia watu mashuhuri wetu tunaowapenda ambao walifichua  kwa umma kwamba walikuwa wameanzisha uhusiano mpya.

Mastaa hao ni pamoja na;

1.Nadia Mukami na Arrow Bwoy

Nadia Mukami, ambaye kwa muda mrefu tangu aingie kwenye muziki alisisitiza kwamba amekuwa hajaolewa kila siku, hivi karibuni aliwashangaza mashabiki wake baada ya kubaini kuwa yuko kwenye uhusiano na mwanamuziki mwenzake Arroy Bwoy.

“Tunachumbiana? Ndio. Nimekuwa mpenzi wa Arrow / Ali kwa muda sasa. Nimekuwa nikichumbiana. Tumekuwa pamoja kwa muda mrefu kuliko vile watu wanaweza kudhani.

2.Rayvanny na Paula Kajala

Rayvanny alithibitisha uhusiano wao katika chapisho la Instagram. Mwimbaji alishiriki picha akiwa amemkumbatia Paula, na wote wawili wakitazama nje kupitia dirishani.

Kwenye ukurasa wake, Paula alishiriki picha hiyo hiyo na kuiandika kwa upendo.

Tangu kuthibitisha uhusiano huo, wawili hao wameonekana hadharani wakifurahiya maisha yao ya mapenzi pamoja.

3.Juliana na LIlian Ng'ang'a

Miezi kadhaa baada ya kudhaniwa kuwa Julius Owino, jina jingine Juliani na Lilian Ng'ang'a, mke wa zamani wa Gavana wa Machakos Alfred Mutua, walikuwa katika uhusiano, mwimbaji huyo amejitokeza kudhibitisha kuwa kweli wao ni kitu kimoja.

4.Ronald Ndubi na Dore Chege

Aliyekuwa muigizaji wa kipindi cha Maria Victoe, akiwa kwenye mahojiano alithibitisha kwamba yuko kwenye uhusiano wa kimapenzi na muigizaji mwenzake maggie.

Pia alifichua kwamba harusi iko njiani.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved