Hivi karibuni mfumo wa elimu wa CBC umekabiliwa na upinzani mkubwa kutoka kwa wazazi na washika dau wa elimu nchini.
Wazazi na waalimu wengi wamejitokeza haswa mitandaoni kutoa malalamiko yao kuhusiana na mfumo huo ambao ulizinduliwa nchini mwaka wa 2017 baada ya kutupiliwa kwa mfumo wa hapo awali wa 8-4-4.
Kufuatia malalamishi hayo, tayari rais wa mawakili nchini Nelson Havi ametangaza kuwa atawasilisha kesi kortini wiki ijayo akipinga mfumo huo ambao haujapokewa vizuri na asilimia kubwa ya Wakenya.
"Nimeskia kilio cha wazazi, walezi na walimu. Kesi ya kupinga CBC itawasilishwa kortini wiki ijayo. Mfumo wa elimu nchini haufai kuwa jaribio ghali, lisiofaa na ambalo halifanyi kazi kwa viongozi wetu wa kesho" Havi aliandika kwenye mtandao wa Twitter mapema wiki hii.
I have heard your cries parents, guardians and teachers. The petition challenging CBC will be filed in Court next week. The education system in Kenya should not be an expensive, inefficient and ineffective experiment with our children and their future as is our leadership. ^DoS
— Nelson Havi (@NelsonHavi) September 8, 2021
Wazazi wengi wamekuwa wakilalamika gharama kubwa ya kutekeleza mfumo huo huku wakiagiza serikali kurejesha mfumo wa zamani wa 8-4-4 ambao haukuwagharimu pesa nyingi.
CBC inawahitaji watoto wao kutumia vifaa vya kiteknolojia kama vile simu, kompyuta na televisheni ambavyo wazazi wamelazimika kuwatafutia watoto wao.
Baadhi ya vifaa hivyo hutumia data ama Wi-Fi ili kufanya kazi, jambo ambalo limewachokesha wazazi wengi ambao wameeleza malalamiko yao kufuatia gharama kubwa ya data na WiFi nchini.
Magoha do you really live in Kenya ? How do you expect a parent who cannot afford food to buy a computer or smartphone for their children ? This CBC nonsense will not work in Kenya! Stop this utopian thinking!!!
— Sen. Ledama Olekina (@ledamalekina) September 10, 2021
Kando na hayo, baadhi ya wazazi wameeleza kuwa wameagizwa kuwanunulia watoto wao vitabu zaidi, hatua ambayo wengi wamehisi imewaacha na mzigo mkubwa mgongoni.
CBC requires me to do all this, I can coz am in town.
— Dan Mwanzia (@DannMwanzia) September 10, 2021
What about my village peers at Mutendeu primary school where a cyber cafe is an alien terminology?#CBCmustFall pic.twitter.com/G21TsyjAml
Sio vitabu pekee kwani mfumo wa CBC unawahitaji watoto kujua kufanya kazi za kinyumbani kama vile kupika, kuosha, kushona n'k. Kufuatia hayo wazazi wanahitajika kunulia watoto wao vitu vinavyohitajika kufanya mafunzo hayo kama vile vyakula na vifaa vya kushona.
Isitoshe, wazazi wengine wamelalamika kuwa wamelazimika kusaidia watoto wao kufanya nyingi kazi za ziada ambazo wamekuwa wakipewa shuleni.
It is curriculum where teachers give assignments to the parents, the children are just cordinators🙄🙄we are suffering#CBCmustFall pic.twitter.com/NI18Q5QcC9
— Collins Misoi KE (@MisoiCollin) September 10, 2021
Nelson Havi should just save our kids from this CBC fraud. This system is worse than 'worser'. #CBCmustFall pic.twitter.com/FLhq8U2RUb
— ACHOLA DICHOL (@NamelokLLB) September 10, 2021
Kwenye mfumo wa CBC wanafunzi wanahitajika kujua namna ya kutengeneza vitu kama vile 'scarecrow', magari ya kuchezea, vifagio miongoni mwa vitu vingine.
Baadhi ya wazazi wanahisi kuwa kazi zile zinachokesha haswa kuona kuwa wanalazimika kuzifanya pamoja na watoto wao mida ya jioni wakati kila mmoja amerejea nyumbani.
Hali hii imewafanya wazazi kutia msukumo kwa serikali itupilie mbali mfumo wa CBC ambao sasa uko katika mwaka wake wa tano.
CBC has engaged parents more than the learner's #CBCmustFall pic.twitter.com/XU4c58XEZR
— Sharim Enock✴️✴️🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪 (@EnockSharim) September 10, 2021
Hata hivyo waziri wa Elimu George Magoha amesisitiza kuwa utaendelea na serikali haina nia ya kuutupilia mbali.