logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Orodha ya viongozi wa kigeni waliohudhuria misa ya hayati Mwai Kibaki katika Nyayo Stadium

•Misa hiyo ilianza mwendo wa saa tano na inatarajiwa kuisha wakati wowote kuanzia saa nane alasiri. •Zaidi ya viongozi 8 wa mataifa ya kigeni ni miongoni mwa wageni waliohudhuria ibada ya kumpungia Kibaki mkono wa buriani.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri29 April 2022 - 11:02

Muhtasari


•Misa hiyo ilianza mwendo wa saa tano na inatarajiwa kuisha wakati wowote kuanzia saa nane alasiri.

•Zaidi ya viongozi 8 wa mataifa ya kigeni ni miongoni mwa wageni waliohudhuria ibada ya kumpungia Kibaki mkono wa buriani.

Misa ya Hayati Mwai Kibaki yaendelea katika uwanja wa Nyayo mnamo Aprili 29,2022

Misa ya mazishi ya rais wa tatu wa Kenya hayati Emillio Mwai Kibaki inaendelea katika uwanja wa Nyayo, jijini Nairobi.

Misa hiyo ilianza mwendo wa saa tano na inatarajiwa kuisha wakati wowote kuanzia saa nane alasiri.

Ibada hiyo ya kitaifa  imehudhuriwa na watu kutoka matabaka mbalimbali na vilevile nchi tofauti.

Rais Kenyatta aliwasili ugani Nyayo mwendo wa saa nne unusu asubuhi na kupokelewa na naibu wake William Ruto.

Zaidi ya viongozi wanane wa mataifa ya kigeni ni miongoni mwa wageni waliohudhuria ibada ya kumpungia Kibaki mkono wa buriani.

Orodha:-

1. Cyril Ramaphosa- Rais wa Afrika Kusini

2. Salva Kirr- Rais wa Sudan Kusini

3. Sahle-Work  Zewde- Rais wa Ethiopia.

4. Edward Ngirete- Waziri Mkuu wa Rwanda

5.  Philip Mpango- Naibu Rais wa Tanzania

6. Constantino Chiwenga- Naibu Rais wa Zibambwe

7. Jesicca Alupo- Naibu Rais wa Uganda

8. Joyce Banda- Aliyekuwa Rais wa Malawi

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa,Rais wa Ethiopia Sahle-Work Zewde,Rais wa Sudan Kusini Salva Kir na Rais Uhuru Kenyatta wakiwa katika uwanja wa Nyayo wakati wa mazishi ya kitaifa ya aliyekuwa Rais Mwai Kibaki Aprili 29,2022

Rais Uhuru Kenyatta alitangaza habari za kifo cha aliyekuwa mtangulizui wake, Mwai Kibaki Ijumaa ya wiki jana.

Siku tatu, Jumatatu, Jumanne na Jumatano zilitengwa kwa umma kuona mwili wa hayati na kumpatia heshima za mwisho.

Hayati atazikwa Jumamosi nyumbani kwake katika eneo la Othaya, kaunti ya Nyeri.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved