•Tume ya IEBC ilimdhinisha Wajackoyah kuwania kiti cha urais pamoja na mgombea mwenza wake Justina Wamae.
•Durag ni kitambaa kinachositiri kichwa ambacho hufungwa ili kuikinga nywele .
Mgombea rais kwa ticketi ya Roots Party of Kenya Prof. George Wajackoyah amefichua kwamba huwa anatumia durag kama ishara ya kupingana na ufisadi nchini Kenya.
Akiwa kwenye mahojiano na runinga ya Citizen tv,Wajackoyah alizungumza kuhusu maisha yake ya kawaida ya awali.
“Nilikuwa chokora na mchimba makaburi,’alisema.
‘ Niko na watoto na bibi ambao wanaishi Merekani, durag ni ishara ya kupigana na ufisadi. Wakati Wamarekani wenye asili ya Kiafrika walikamatwa na kufungwa,wengi wao walikufa wakiwa kwenye mashua ,mili yao ilitupwa baharini. Kabla ya kuwatupa baharini, walivua nguo za wafu nakuwafunga durag vichwani mwao, idadi ya durag ilikua inaonyesha idadi ya wafu’
Durag ni kitambaa kinachositiri kichwa ambacho hufungwa ili kuikinga nywele .
Wajackoyah alisema, hayuko tayari kuacha kuvalia durag,alisema anahisi vizuri akiwa amevalia vazi hilo.
‘Napenda huu mtindo ya mavazi, niko na suti lakini nahisi vizuri nikiwa kwa mavazi ya kawaida.’
Tume ya IEBC ilimdhinisha Wajackoyah kuwania kiti cha urais pamoja na mgombea mwenza wake Justina Wamae.
Wawili hao walipata nafasi ya kuonyesha wapiga kura kuhusu ukulima wa bangi kama kitega uchumi. Alisema kwamba atazindua manifesto yake mnamo Julai 2 mwaka huu.