• Wizara ya Afya nchini Kenya imekiri kwamba homa na saratani ya ini ni tatizo kubwa nchini.
• Kufuatia mkurupuko wa janga la Covid-19 raslimali nyingi katika idara ya afya zilielekezwa kufadhili kampeini dhidi ya Covid-19.
Shirika hilo limeelezea umuhimu wa kuimarisha huduma za matibabu kwa umma ikiwemo kuleta karibu na wananchi vituo vya matibabu ili kusaidia katika vita dhidi ya ugonjwa huu hatari. Linalenga kupunguza kiwango cha homa ya ini aina za B na C kwa asilimia 90, kupunguza vifo vinavyohusishwa na saratani ya ini kwa asilimia 65 na kuhakikisha kwamba takribani asilimia 90 ya walioambukizwa wanapata matibabu bora.
Kenya ni miongoni mwa mataifa ambayo raia wake wanakumbwa na hatari ya kuambukizwa homa ya ini. Kulingana na hospitali ya Aga Khan [AKUH], pindi tu mtu anapoambukizwa na virusi hivi, mwili hushindwa kuifadhi joto na kutoa uchafu mwilini.
Umaskini pia umechangia pakubwa katika kuongezeka kwa idadi ya maafa yanayotokana na ugonjwa huu. Kulingana na Christopher Baraza ambaye alipoteza ndugu kutokana na homa ya ini, ukosefu wa matibabu kutokana na hali ya kutomudu gharama za matibabu kumechangia vifo vingi.
Christopher anasema baada ya nduguye kuambukizwa, ilikuwa vigumu kwao kumtafutia matibabu kwani familia yake tayari ilikuwa inakabiliwa na changamoto za kukimu mahitaji ya kimsingi.
Kutokana na hali hii, Christopher alimpoteza nduguye kwa ugonjwa wa saratani ya ini baada ya juhudi za kusaka wahisani kufeli.
Wizara ya Afya nchini Kenya imekiri kwamba homa na saratani ya ini ni tatizo kubwa nchini hasa kufuatia mkurupuko wa janga la Covid-19 ambapo raslimali nyingi katika idara ya afya zilielekezwa kukabili Covid-19.
Katika maadhimisho ya siku hii shirika la WHO linakumbusha mataifa kuzidisha juhudi za kukabili ugonjwa wa homa ya ini.
wananchi wanataadharishwa dhidi ya kupuuza dalili za ugonjwa huu kwa kutembelea vituo vya afya kupimwa na kupokea matibabu.