Je, dunia inaweza kubeba watu wangapi?

Idadi ya binadamu duniani kwa sasa inafikia 9.4 bilioni hadi 10.4 bilioni.

Muhtasari

•Makadirio yanatofautiana, lakini inatarajiwa kwamba idadi ya watu duniani itafikia kilele chake cha hesabu kati ya 2070 na 2080.

Image: BBC

Ni miaka 72,000 kabla ya Kristo wakati volkeno kubwa iitwayo Toba, iliyo katika kisiwa cha Indonesia cha Sumatra, ililipuka. Ilichukuliwa kuwa tukio kubwa zaidi duniani katika miaka mia moja iliyopita.

Matokeo yake, eneo kubwa la bara Asia lilikuwa vumbi lenye unene wa sentimita 3-10.

Baadhi ya wanasayansi wanaamini kwamba hii ilisababisha dunia kuingia katika volkeno ambayo ilidumu kwa miongo kadhaa na karibu isababishe kutoweka kwa jamii ya binadamu.

Utafiti umeonyesha kuwa tukio hilo lilitokea kati ya miaka 50,000 na 100,000 iliyopita.

Wakati huo, jumla ya idadi ya watu duniani ilikuwa ndogo karibu watu 10,000 tu.

Baadhi ya wataalam wanaamini hii si tu ajali. Kulingana nao, wanaamini kuwa mlipuko wa volkeno ya Toba ndio uliofanya hivyo.

Wazo hilo linapingwa vikali, lakini hakuna shaka kwamba sehemu kubwa ya binadamu imetokana na idadi ndogo ya watu wenye nguvu sana.

Nyakati fulani, wakazi wa maeneo yote ya dunia wamekuwa katika hatari kubwa.

Na kuthibitisha miaka 74,000 aina zetu za nyani wasiokuwa na manyoya ambao wamepitia mlipuko wa idadi ya watu, wakikoloni karibu kila makazi kwenye sayari na kutoa ushawishi wetu kwenye pembe za mbali zaidi - mnamo 2018, wanasayansi walipata mfuko wa plastiki 10,898m (35,754 ft. ) chini ya uso wa bahari chini ya Mfereji wa Mariana, wakati timu nyingine hivi majuzi iligundua ‘’kemikali za milele’’ zinazotengenezwa na binadamu kwenye Mlima Everest.

Hakuna sehemu ya ulimwengu iliyo safi - kila ziwa, msitu na korongo zimeguswa na shughuli za wanadamu.

Wakati huo huo, idadi yetu kamili na ustadi umewezesha wanadamu kufikia mambo ambayo hakuna mnyama mwingine angeweza kuota - kugawanya atomi, kutuma vifaa vigumu karibu maili milioni (kilomita milioni 1.6) kutazama sayari zikiundwa katika galaksi za mbali, na kuchangia utofauti mkubwa wa sanaa na utamaduni.

Kila siku, kwa pamoja tunapiga picha bilioni 4.1 na kubadilishana kati ya maneno trilioni 80 na 127.

Katika tarehe maalum isiyo ya kawaida ya tarehe 15 Novemba 2022, Umoja wa Mataifa umetabiri kwamba idadi ya binadamu walio hai duniani itaongezeka na kufikia bilioni 8 kwa wakati mmoja, idadi ambayo itakuwa ni mara 800,000 zaidi ya wale walionusurika katika janga la Toba.

Leo, idadi ya watu wetu ni kubwa sana, huku kukiwa na tofauti ndogo sana za DNA – nje ya Afrika – mtafiti mmoja hivi majuzi aliona haishangazi kwamba baadhi ya watu wanafanana sana na watu wasiowafahamu kabisa – kuna kundi dogo la DNA ambalo linarejelewa kila mara (katika umbo la watoto wanaozaliwa) kwa matukio haya ya kijeni ambayo hutokea kila siku.

Lakini kwa kuongezeka kwa idadi ya watu kumekuja na mgawanyiko mkubwa.

Wengine wanaona nambari zetu zinazoongezeka kama hadithi ya mafanikio ambayo haijapata kushuhudiwa - kwa kweli, kuna mawazo yanayoibuka ambayo kwa kweli tunahitaji watu zaidi.

Mnamo mwaka wa 2018 bilionea wa teknolojia Jeff Bezos alitabiri siku zijazo ambapo idadi ya watu itafikia hatua mpya ya desimali, wanadamu trilioni waliotawanyika katika Mfumo wetu wa Jua - na akatangaza kwamba anapanga njia za kufanikisha hilo.

Mwanahistoria wa masuala ya matangazo na mazingira wa Uingereza Sir David Etonbra, kwa upande mwingine, anaelezea ongezeko la idadi ya watu ambalo halikutegemewa kuwa ni "pigo kwa dunia".

Anaamini kwamba ongezeko hilo limechangia kila tatizo la mazingira linalomkabili mwanadamu leo, kama ni mabadiliko ya hali ya hewa, kutoweka kwa mimea mbalimbali, maji na migogoro juu ya ardhi na mabishano mengine juu ya mali nyingine za asili.

Mwaka 1994, wakati jumla ya idadi ya watu duniani ilikuwa bilioni tano na nusu, Chuo Kikuu cha Stanford katika California, jimbo la Marekani, kilifanya hesabu na kusema kwamba idadi bora ya watu duniani ni kati ya bilioni 1.5 na 2.

Kwa hivyo ulimwengu umejaa watu wengi kwa sasa?

Na nini kinaweza kutokea wakati wa siku za usoni kwa binadamu kimataifa?

Mjadala kuhusu idadi inayofaa ya watu kwenye sayari limekuwa nyeti sana - lakini wakati unaendelea kuyoyoma katika kuamua ni mwelekeo gani bora.

Wasiwasi wa zamani

Ilikuwa mwishoni mwa miaka ya 1980 katikati mwa Iraq, na timu ya wanaakiolojia kutoka Chuo Kikuu cha Baghdad walikuwa wakichimba vitu vya kale.

Walipata mabamba 400 ya udongo - rekodi ambazo zilikuwa zimesahauliwa katika kaburi lao la kitaaluma kwa zaidi ya miaka elfu tatu na nusu, kutoka kwenye eneo la karamu katikati ya Iraq, kipindi cha Babeli ya zamani.

"Miaka 1200 ilikuwa bado haijapita [tangu kuumbwa kwa wanadamu], Wakati nchi ilipoenea na watu wakaongezeka ... "kulingana na Atra-hasis - shairi kuu lililowekwa muhuri kwenye udongo na mwandishi asiyejulikana karibu na Karne ya 17 KK.

Katika hadithi ya zamani, inasemekana miungu hukasirishwa na "kelele" na "kelele" zote zinazosababishwa na mwanadamu, na vile vile "ardhi inayotoa sauti nzito kama fahali" kwa sababu ya misongo ya mawazo ambayo walipitia kutokana na mahitaji ya spishi zetu.

Mungu wa angahewa, Enlil, akaamua kuachilia hatari chache ili kupunguza idadi tena - kuleta majanga, njaa na ukame kupiga kwa vipindi vya kawaida vya miaka 1,200.

Na wakati huu, kwa bahati nzuri, mungu mwingine akaokoa.

Lakini Enlil akapanga mafuriko makubwa badala yake... na hadithi ya kawaida ya ujenzi wa mashua inafuata.

Inakadiriwa kwamba wakati habari hii ilipokuwa ikiandikwa, idadi ya watu duniani ingekuwa kati ya milioni 27 na 50 idadi hii ikiwa ni sawa na watu wanaoishi Cameroon au Korea Kusini au 0.3-0.6% ya jumla ya wale wanaoita sayari nyumbani hii leo.

Wakati wa milenia iliyofuata, wasomi wanaonekana kuwa kimya juu ya wasiwasi wowote wa idadi ya watu.

Kisha katika Ugiriki ya Kale, wakaanza kutafakari suala hilo tena.

Mwanafalsafa Plato alikuwa na maoni fulani yenye nguvu.

Baada ya kipindi cha ukuaji wa haraka, ambapo idadi ya watu wa Athene iliongezeka maradufu, alilalamika: "Kilichosalia sasa ni kama mifupa ya mwili iliyoharibiwa na ugonjwa; udongo wenye rutuba umechukuliwa na jina tu ndio lililosalia."

Sio tu kwamba aliamini katika udhibiti mkali wa idadi ya watu, unaosimamiwa na serikali - hatimaye alihitimisha kuwa jiji linalofaa haipaswi kuwa na zaidi ya raia 5,040, na alifikiri kuanzisha makoloni ilikuwa njia nzuri ya kupunguza ziada yoyote - lakini pia aliona umuhimu wa kudhibiti matumizi.

Katika maandishi ya Plato, yaliyoandikwa karibu miaka 375KK, anaelezea miji miwili ya kufikirika - mikoa ya kiutawala inayotawaliwa mfano wa nchi ndogo.

Moja kuna "afya" na kwingine ni "anasa".

Mwishoni, idadi ya watu huwa na matumizi kupita kiasi, hadi "wanavuka kikomo cha mahitaji yao".

Hata hivyo, jimbo hili la jiji lililoshuka kimaadili hatimaye linaamua kunyakua ardhi jirani, na kama kawaida kuingia kwenye vita - haliwezi kuendeleza idadi yake kubwa ya watu wenye pupa au ulafi bila rasilimali za ziada.

Plato alikuwa amezua mjadala ambao bado unaendelea hadi leo: je, idadi ya watu ndiyo suala lenyewe, au ni rasilimali inayotumiwa?

Ilichukua zaidi ya karne tano baada ya Plato kabla ya kiwango cha kimataifa cha mlipuko wa idadi ya watu kuwa wazi.

Mwandishi Tertullian, aliyeishi katika jiji la Kirumi la Carthage huko Roma, alitoa maoni ya kisasa kuhusu umati wetu na uharibifu miaka ya sasa.

Mnamo 200AD, wakati jumla ya idadi ya watu ilikuwa imefikia milioni 190-256 - karibu na idadi ya watu wanaoishi Nigeria au Indonesia kwa sasa - aliamini kwamba ulimwengu wote ulikuwa tayari umegunduliwa, na watu wamekuwa mzigo kwenye sayari maana asili haiwezi tena kutudumisha…

Katika miaka 1,500 iliyofuata, idadi ya watu duniani iliongezeka zaidi ya mara tatu.

Hatimaye, wasiwasi huu uliojitenga uligeuka kuwa hofu.

Katika kazi yake maarufu, insha yenye kuangazia kanuni ya Idadi ya Watu, iliyochapishwa mwaka wa 1798, alianza na chunguzi mbili muhimu - kwamba watu wote wanahitaji kula, na wanapenda kufanya ngono.

Wakati kuchukuliwa kwa hitimisho lao la kimantiki, alielezea, ukweli huu rahisi kuwa hatimaye kungesababisha mahitaji ya binadamu kushindwa kwendana na vilivyomo kwenye sayari.

Maneno haya rahisi yalikuwa na athari ya papo hapo, yakizua hofu ya shauku kwa wengine na hasira kwa wengine, ambayo ingeendelea kusikika katika jamii kwa miongo kadhaa.

Wa kwanza walidhani kwamba kuna kitu kinapaswa kufanywa ili kuzuia idadi yetu kuongezeka bila kudhibitiwa.

Mwishowe, ilichukuliwa kuwa kuweka kikomo idadi ya watu ilikuwa ni upuuzi au kinyume cha maadili, na kila juhudi inapaswa kufanywa kuongeza usambazaji wa chakula badala yake.

Kambi ya watu wachache ilikosoa Sheria Duni za Kiingereza zilizoanzishwa mamia ya miaka iliyopita, ambayo ilihusisha malipo kwa wale wanaoishi katika umaskini ili kuwasaidia kutunza watoto wao.

Ilikisiwa kuwa haya yalihimiza watu kuwa na familia kubwa.

Wakati hadithi ya Malthus ilichapishwa, kulikuwa na watu milioni 800 kwenye sayari.

Haikuwa hadi 1968, hata hivyo, wasiwasi wa kisasa kuhusu kuongezeka kwa idadi ya watu ulimwenguni uliibuka wakati profesa katika Chuo Kikuu cha Stanford, Paul Ehrlich, na mkewe, Anne Ehrlich, waliandika pamoja kitabu cha "The Population Bomb."

Mji wa India wa Delhi ulikuwa na hamasa.

Walikuwa wakirejea hotelini kwao wakiwa kwenye teksi jioni moja na kupita kwenye kitongoji duni, ambapo walizidiwa na shughuli nyingi za kibinadamu mitaani.

Waliandika kuhusu uzoefu wao kwa njia ambayo imekosolewa vikali - hasa kwa vile wakazi wa London wakati huo walikuwa zaidi ya mara mbili ya Delhi.

Wanandoa hao waliandika kitabu chao kwa sababu ya wasiwasi juu ya njaa kubwa ambayo waliamini inakuja, haswa kwa nchi zinazoendelea - lakini pia katika maeneo kama Marekani, ambapo watu walianza kugundua athari waliyokuwa nayo kwa mazingira.

Bila shaka, majadiliano kuhusu watu wangapi wanapaswa kuwapo hayajawahi kuwa ya kitaaluma tu.

Wakati fulani, wametekwa nyara ili kuhalalisha mateso, mauaji ya kikabila na mauaji ya kimbari.

Mapema mwaka wa 1834, miongo mitatu na nusu tu baada ya maneno ya Malthus kuchapishwa, Sheria Duni za Kiingereza zilitupiliwa mbali na badala yake zikawekwa sheria kali zaidi.

Hili kwa kiasi fulani lilitokana na wasiwasi wa Wamalthus kwamba tabaka hili la kati (lililojulikana kama wakulima wadogo) lilikuwa likizaliana sana, na matokeo yake ilikuwa kuwalazimisha watoto yatima kwenye nyumba zisizo na mazingira bora kiafya, zisizo safi kama ile iliyoonyeshwa katika riwaya ya ‘’Charles Dickens ya Oliver Twist.’’

Katika karne zijazo, mambo yakaendelea kubadilika hadi kufikia kiwango cha kulazimishwa kufunga uzazi kwa watu kutoka makabila madogo katika miaka ya 1970 nchini Marekani.

Pia ilitumika kupunguza uhuru wa mtu binafsi.

Mwaka 1980, China ilianzisha sera yake yenye utata ya mtoto mmoja, ambayo ilionekana sana kama ukiukwaji wa haki za ngono na uzazi.

Mustakabali tata

Siku hizi, kuna ukosoaji mkubwa wa malengo yote na sera zinazohusiana na upendeleo zilizowekwa kwa ajili ya kupunguza au kuongeza idadi ya binadamu, lakini kinyume chake, pia kuna maoni kwamba idadi ya watu inaweza kudhibitiwa kwa njia za hiari, kama vile utoaji wa huduma za kuzuia mimba.

Baadhi ya wataalamu wanaamini kwamba suluhisho halipo katika kuwashinda au kuongeza idadi ya watu bali katika usambazaji wa haki na matumizi ya rasilimali.

Wanasema kwamba katika nchi tajiri ambapo kiwango cha kuzaliana ni kidogo lakini kwa matumizi ya rasilimali ni kubwa zaidi kuliko katika nchi masikini.

Baadhi ya watu pia wanasema kwamba upendeleo wa rangi uko nyuma ya idadi ya watu katika nchi masikini kwa sababu nchi zilizoendelea zina idadi kubwa ya watu.

Baadhi ya wataalam hawana haja ya kufanya chochote kuhusu idadi ya watu. Wanafikiri idadi ya watu itaongezeka kivyovyote vile, lakini baadaye itaanza kupungua na kila mtu atapata kile anachotaka kupata.

Makadirio yanatofautiana, lakini inatarajiwa kwamba idadi ya watu duniani itafikia kilele chake cha hesabu kati ya 2070 na 2080, na idadi ya binadamu duniani kwa sasa inafikia 9.4 bilioni hadi 10.4 bilioni.