logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Idadi ya waliofariki Morocco kwa zilizala yazidi 2000, je, ni nini husababisha zilizala?

• Tetemeko la ardhi husambabisha maafa mengi duniani kwa misimu tofauti

image
na

Habari11 September 2023 - 04:45

Muhtasari


• Kulingana na wasomi wakuu wa maswala yanayohusiana na maswala ya tetemeko la ardhi ni kuwa hatuwezi kuzuia tetemeko la ardhi.

• Mtetemeko wa ardhi hutokea popote duniani ,wakati wowote wa mwaka kwa hakika haiwezekani kuamua ni wapi na ni lini.

 Wengi hujiuliza tetemeko la ardi ni nini? Hili hapa jibu lake,

Tetemeko la ardhi ni jambo asili na ambalo hutajwa kwa uharibifu mwingi wa mali kwa kuwa hutokea kwa kasi sana bila kutarajiwa.

Tetemeko hili hutajwa kuletwa na milipuko ya volcano ambayo husababishwa na milipuko ya chini ya ardhi.

Kulingana na historia ya dunia kuwa sahani za tectonic daima zinasonga polepole lakini hukwama kwenye kingo zao kwa sababu ya msuguano.

Kuna tetemeko la ardhi ambalo hutoa nishati katika mawimbi ambayo husafiri kupitia ukanda wa dunia na kusababisha kutetemeka  tunayohisi.

Fahamu kuwa tetemeko kuu duniani 7.0-7.9 na inaweza kusababisha uharibifu mkubwa duniani

Kulingana na wasomi wakuu wa maswala yanayohusiana na maswala ya tetemeko la ardhi ni kuwa hatuwezi kuzuia tetemeko la ardhi bali tunaweza kuzuia au kupunguza madhara yake kwa kutoa elimu kuhusu usalama wa tetemeko la ardhi.

Mtetemeko wa ardhi hutokea popote duniani ,wakati wowote wa mwaka kwa hakika haiwezekani kuamua ni wapi na ni lini na jinsi tetemeko la ardhi litakuwa na nguvu.

Mara mingi tetemeko la ardhi linapotoke husababisha majumba mengi kuanguka na pia milipuko mikubwa husababisha sehemu mbalimbali kutenganishwa huku watu wengi huachwa bila nyumba na pia magojwa mbalimbali hutokea wakiwemo watu wengi kuwa walemavu na mayatima.

Je? kunapotokea tetemeko la ardhi unapaswa kufanya nini. Haya ni baadhi ya mambo ya kuzingatia katika tukio la tetemeko la ardhi ,lakini suala la msingi ni linalosisitizwa na wataalamu ni kutulia .

 Wakati wa tetemeko la ardhi hupaswi kukimbia kwani ni hatari kwa usalama wako mbali unafaa kutulia ulipo na kutafuta njia za kutoka ikiwa kunazidi kuwa na hatari unapaswa kuwajuza maafisa wa vikosi vya mikasa ya mlipuko wa ardhi.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved